logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Chipukeezy avunja kimya siku chache baada ya kulazwa hospitali

Alipigwa picha akitumia muda katika moja ya mashamba yake.

image

Burudani04 August 2023 - 12:30

Muhtasari


  • MC wa Ikulu ameshiriki picha kwenye akaunti yake rasmi ya mtandao wa kijamii na kuwafahamisha Wakenya kuhusu afya yake.

Vincent Mwasia Mutua, maarufu kwa jina la kisanii Chipukeezy, Mchekeshaji maarufu wa Kenya na Mc wa Ikulu amevunja ukimya siku chache baada ya kulazwa katika Hospitali ya Nairobi West kutokana na ugonjwa ambao haujajulikana.

MC wa Ikulu ameshiriki picha kwenye akaunti yake rasmi ya mtandao wa kijamii na kuwafahamisha Wakenya kuhusu afya yake.

Katika picha Chipukeezy alionekana dhaifu kidogo. Hata hivyo amewahakikishia Wakenya kwamba anaendelea kupata nafuu.

"Katika safari ya maisha, afya ni hazina kuu. Ninaendelea vyema katika kupona kwangu na tunamshukuru Mungu" aliandika Chipukeezy kwenye akaunti zake rasmi za mitandao ya kijamii.

Mchekeshaji huyo alitoa habari hizo njema kwenye mtandao wake rasmi wa kijamii wa Instagram akiwahakikishia mashabiki wake kuwa anaendelea vizuri na kwamba ameruhusiwa kutoka Hospitali.

Alipigwa picha akitumia muda katika moja ya mashamba yake.

Haya yanajiri siku chache baada ya kulazwa hospitalini. Dennis Itumbi, mmoja wa washirika wake wa karibu alikuwa amefichua kuwa Chipukeezy alikuwa na matatizo ya kiafya ambayo yalikuwa bado yanafanyiwa majaribio wakati huo na hivyo kusababisha kulazwa hospitalini.

Chipukeezy alikuwa na onyesho kubwa lililokusudiwa kufanywa tarehe 5 Agosti na ambalo lingehudhuriwa na watu mashuhuri akiwemo binti wa kwanza Charlene Ruto.

Hata hivyo iliahirishwa kutokana na suala la Afya.

Mashabiki walimtakia afueni ya haraka na hizi hapa baadhi ya jumbe zao;

tomdaktari: Itakua sawa

timo: Quick recovery kasee @chipukeezy

thepositivethinker: It will be well Bro, Solidier on.....

lilian: Get well soon Chipu.

washington: quick recovery

edwin: Quick recovery mzee Chipuuu πŸ™

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logoΒ© Radio Jambo 2024. All rights reserved