logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Maua Sama na Zuchu waparurana mitandaoni kisa madai ya kununua views YouTube

Wasanii hao wamekuwa wakipapurana bila kutajana kwa majina.

image
na Radio Jambo

Burudani07 August 2023 - 07:40

Muhtasari


• Mwaka jana, msanii Harmonize alisutwa vikali kwa kile kilisemekana kwamab ni kununua views kwa ajili ya wimbo wake aliomshirikisha msanii wake Ibraah kwa jina mdomo.

Maua Sama na Zuchu waparurana.

Siku chache baada ya Zuchu kudai kwamba wasanii wa Bongo Fleva wengi wanaishi kwa kununua utazamaji kwenye jukwaa la YouTube, msanii mwenzake wa kike Maua Sama ameonekana kumjibu.

Kupitia Twitter yake, Maua Sama anadai kwamba Zuchu naye ni mmoja wa wanaonunua views lakini sasa amefikia hatua ya kuwaonea wenzake wanaonunua kama yeye wivu.

Zuchu alikuwa amezua kwamba wasanii wengi wa Tanzania wanaishi maisha ya kuigiza kujidanganya kwamba wanaweza fikisha utazamaji Zaidi ya milioni kwenye nyimbo zao YouTube hali ya kuwa wananunua utazamaji huo.

“Nawaza kama msanii unasikia aje kununua viewrs? Ni kama unajijua nafasi yako ila ndio hivyo tena unaficha kimoyo moyo, unajisikia aje yaani,” Zuchu alisema.

Sama kwa jibu lake, alidokeza kwamba Zuchu naye ni mmoja wa wategemezi wakubwa wa robot za kuongeza views ghushi akisema kwamab ameanza kuwaonea wenzake wivu.

“Maisha haya, marobot wamenza kuoneana wivu,” Maua Sama aliandika.

Japo Sama hakumtaja Zuchu, watu wengi kwenye maoni waliona hilo ni jibu la moja kwa moja kwa Zuchu ambaye aliibua wasiwasi wake kuhusu baadhi ya wasanii wa Bongo kununua views, ambapo pia naye hakumtaja mtu.

Tasnia ya muziki wa Bongo katika miaka ya hivi karibuni imekuwa ikigubikwa na madai kama hayo ya ununuzi wa views mitandaoni, madai ambayo hata hivyo hayajapata kuthibitishwa.

Mwaka jana, msanii Harmonize alisutwa vikali kwa kile kilisemekana kwamab ni kununua views kwa ajili ya wimbo wake aliomshirikisha msanii wake Ibraah kwa jina mdomo.

Wimbo huo ndani ya saa moja baada ya kuachiliwa, ulikimbia na kupata watazamaji Zaidi ya milioni 1.5 ghafl, jambo ambalo lilitajwa na wengi kuwa si la kawaida na wengine wakisema kuwa ni rekodi ambayo haikuwahi kuonekana tena.

Kilichowashangaza wengi ni wimbo huo kuanza kujikokote katika siku za baadae na kumaliza mwezi ukiwa na watazamaji wasiozidi milioni 2.5, licha ya kupata utazamaji milioni 1.5 ndani ya saa moja.

Je, unaamini wasanii wa Bongo wako chini ya shinikizo la kila mmoja kutaka kuonekana kuwa na utazamaji mwingi kwenye YouTube kiasi kwamba wanaishia kununua views?

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved