logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Khaligraph Jones amtaja Octopizzo kama model wa Instagram

“Anafanya kazi nzuri, ana kurasa safi sana kwenye mitandao ya kijamii."

image
na Radio Jambo

Burudani15 August 2023 - 09:50

Muhtasari


• Hata hivyo, Khaligraph alimchimba mkwara Octopizzo akimlinganisha kama mwanasosholaiti wa Instagram ambaye anafanya vizuri kwa upande huo.

Khaligraph Jones na Octopizzo.

Kwa mara nyingine tena, rapa Khaligraph Jones amezungumzia kuhusu ‘uadui’ wa kimuziki baina yake na rapa mwingine Octopizzo.

Akizungumza na Obinna, Khaligraph alisema kwamba yeye hana tatizo wala chui dhidi ya Octopizzo ila Octopizzo ndiye kama hampendi tu na wala hawezi kumlaumu kwa kumchukia.

Alisema kwamba yeye kwa sasa amefikisha umri wa miaka 33 na hana muda wa kuhasimiana na Octopizzo akisema kuwa wakati wowote akimkuta analazimisha kusalimiana naye bila kujali kama ataitikia salamu au la.

“Huyo mvulana hajawahi nipenda, unajua kuna tu mtu unahisi kama huwezi mpenda na huwezi mlaumu, ulizaliwa tu hivyo. Niliona kwa mahojiano akisema kwamba hanipendi vile ninavaa. Mimi namuelewa kwa sababu mimi sihisi kama mimi nahisi hivyo kuhusu mtu mwingine yeyote, lakini namuelewa kwa sababu hata ningekuwa yeye singependa Khaligraph,” alisema.

“Mimi sina uhasama na yeye, sina huo muda ukiona nimefikisha umri wa miaka 33, sasa vitu tulianza huko nyuma mpaka sasa hivi ni wapi na wapi, mimi nikikutana na Octo namsalimia ‘niaje’ akitaka aitike akitaka asiitike mimi nishamsalimia,” Khaligraph aliongeza.

Hata hivyo, Khaligraph alimchimba mkwara Octopizzo akimlinganisha kama mwanasosholaiti wa Instagram ambaye anafanya vizuri kwa upande huo.

“Anafanya kazi nzuri, ana kurasa safi sana kwenye mitandao ya kijamii. Octo ni mwanamitindo mzuri sana, anapiga modelling fiti sana na namheshimu sana kwa kazi hiyo. Jamaa alikuja kutoka Kibera na namheshimu sana kwa sababu alikuja kutoka mazingira magumu sana lakini mambo ya nani anajua kurap kushinda mwingine hiyo tuache,” Khaligraph alisema.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved