logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kabla ya Willis Raburu, mimi ndio nilikuwa mwanzilishi wa shoo ya 10/10 - 2Mbili afichua

“Tuliambiwa tungoje kodogo kidogo tukamuona Willis Raburu akiongoza shoo "

image
na Radio Jambo

Yanayojiri19 August 2023 - 10:02

Muhtasari


• Mchekeshaji huyo ambaye pia ni mkuza maudhui alisema hata hivyo kwamba anawaamini na uwakubali walioteuliwa.

2Mbili asema ndio alianzisha 10Over10

Mchekeshaji 2Mbili amefichua ukweli ambao wengi hawakuwa wanajua kuhusu shoo ya vijana kwenye runinga ya Citizen, 10 over 10.

Katika mahojiano na SPM Buzz, 2Mbili alifunguka sababu yake ya kutoitwa kwenda kufanya usaili wa kuvivaa viatu vikubwa vilivyoachwa na aliyekuwa mwongozaji wa kipindi hicho Willis Raburu.

2Mbili alikiri kwamba kweli hakuitwa kwenda kufanya usaili lakini akafichua kwamba wasichojua wengi ni kwamba yeye ndiye alikuwa mwanzilishi wa shoo hiyo kabla hata Willis Raburu kuikabidhiwa.

“Ambacho watu hawajui ni kwamba mimi ndio nilikuwa mmoja wa waanzilishi wa shoo ya 10 over 10 kabla hata haijaanza kwenda hewani. Mimi JB Masanduku na Fish ndio tuliianzisha mwaka 2016. Tulialikwa Royal Media na sisi ndio tulianzisha kabla hata ujio wa Willis Raburu,” 2Mbili alisema.

Akizungumzia ilikuwaje mpaka hawakuendelea kuiongoza shoo hiyo na badala yake ikapewa kwa Willis Raburu, 2Mbili alisema;

“Tuliambiwa tungoje kodogo kidogo tukamuona Willis Raburu akiongoza shoo hiyo. Lakini bado mimi najivunia kwa sababu nimewahi kuwa mmoja wa hiyo shoo ikiwa ni ya awali kabisa,” alisema.

Mchekeshaji huyo ambaye pia ni mkuza maudhui alisema hata hivyo kwamba anawaamini na uwakubali walioteuliwa ili kuwania nafasi hiyo iliyoachwa wazi na Raburu mwezi mmoja uliopita.

“Lakini bado orodha ya wale walioitwa pale mimi badi nawaaminia wanaweza. Mimi sijaona mtu yeyote pale ambaye naweza sema kwamba naweza bishana na yeye. Nimeona kina Obinna, Kamene na wengine lakini namkubali Gudah Man,” 2Mbili alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved