logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nikianza kutumbuiza nilikuwa natumia chupa za maji kama maikrofoni - Mbosso

"Tulianza nikiwa miaka 16 mpaka sasa hivi nakaribia miaka 28 sio mchezo,” Mbosso alifichua.

image
na Radio Jambo

Makala21 September 2023 - 06:04

Muhtasari


• Msanii huyo alikumbuka kwamba wakati Mkubwa Fella anawafunza jinsi ya kutumbuiza, alikuwa anawapa chupa za maji.

Mbosso.

Mbosso Khan kwa mara ya kwanza amefunguka jinsi alivyoanza safari yake ya muzki mikononi mwa mdau mkubwa sana wa muziki nchini Tanzania ambaye anamuita kama babake katika Sanaa, Mkubwa Fella.

Akizunugumza baada ya mafanikio makubwa ya shoo yake ya mkoa wa Songea alipoingia jukwaani aliwa amejifunga taulo, Mbosso alisema kwamba mafanikio yake yote hayatokani na Wasafi bali ni kwa Mkubwa Fella ambaye ndiye mtu wa kwanza kukitambua kipaji chake na kumpa nafasi ya kukionesha kwa ulimwengu.

“Mkubwa Fella ni baba wa kazi mimi amenilea na amenikuza. Ni mwalimu aliyenifunza muziki. Kwa hiyo mpaka leo hii unauona Mbosso, ni Mkubwa Fella kwanza ndio kafika kwa Mbosso. Akiniona ninatumbuiza, nafanya vizuri, yeye hanioni kuanzia pale mnakoniona nyinyi, ananiona kuanzia steji yangu ya kwanza ya kukua,” Mbosso alisema.

Msanii huyo alikumbuka kwamba wakati Mkubwa Fella anawafunza jinsi ya kutumbuiza, alikuwa anawapa chupa za maji kuzitumia kama vipaza sauti na baadae akawapaisha kutumbuiza kwa umati mdogo mdogo bila maikrofoni.

“Mkubwa alikuwa anatupa chupa za maji hizi unazoziona, alikuwa anatupa unatumbuiza Mkubwa anakuangalia unavyotupa mikono kushoto na kulia, kuwa mtumbuizaji, tukaendelea tukawa paka tukapata vifaa vya bendi tukaanza kutumbuiza bila maikrofoni. Tulianza nikiwa miaka 16 mpaka sasa hivi nakaribia miaka 28 sio mchezo,” Mbosso alifichua.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved