logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mimi napenda wanaume mashoga ambao ni wakonde - Brian Chira afunguka waziwazi

Chira anayeonekana kuwa mlevi alitoa tamko hilo wakati wa kipindi cha moja kwa moja kwenye TikTok.

image
na Davis Ojiambo

Burudani22 September 2023 - 11:23

Muhtasari


  • • Katika video moja ambayo imeibuka ya tiktoker huyo akizungumza kwenye ukurasa wake wa TikToker.
Brian Chira.

TikToker mwenye utata mwingi Brian Chira amerudi na madai mengine yenye ukakasi akidai kwamba yeye anapenda sana wanaume mashoga ambao ni wembamba Zaidi.

Katika video moja ambayo imeibuka ya tiktoker huyo akizungumza kwenye ukurasa wake wa TikToker, anaonekana akikiri waziwazi mapenzi yake kwa wanaume mashoga ila akasisitiza kwamba wale wakonde ndio sampuli yake.

Chira anayeonekana kuwa mlevi alitoa tamko hilo wakati wa kipindi cha moja kwa moja kwenye TikTok.

“Mi napenda wanaume wakonde kama upuuzi. Baba T naona mtado enjoy ndiyo nataka. Ati nisichome, si akuje hapa Baba T, mwite tupambane hapa kwa mtandao,” alisema huku waliojiunga na kikao hicho cha moja kwa moja wakimuonya dhidi ya kumdharau Baba Talisha, mpiga picha maarufu na TikToker, kwani alimsimamia alipokuwa kwenye matatizo.

Tamaa ya Chira kwa wanaume wembamba inakuja miezi miwili tu baada ya kukiri kwamba yeye si shoga. Akiwa na kipindi cha haraka na Mpasho, Chira alisema hiyo ni dhana potofu ambayo watu wanayo juu yake.

"Ni maoni gani potofu ya kawaida juu yako?" mahojiano yalifanywa.

"Kwamba mimi ni shoga," Chira alijibu.

“Je, wewe si shoga?” alizidi kuulizwa na Chira akasema, "Hapana."

TikToker huyo ambaye pia ni mwanafunzi katika Chuo Kikuu cha Kabarak aliangazia zaidi suala la jinsia yake wakati wa mahojiano na mcheshi Oga Obinna mnamo Agosti. Alifichua kuwa anajifanya shoga kwa sababu maudhui yake Wakenya wanataka kula.

“Ndiyo niko sawa. Kwa nini Eric Omondi avae nguo na itakuwa sawa? Mimi ni sawa sana, kuiweka kwenye kumbukumbu. Ni maudhui yake tu. Kwa kuwa hicho ndicho ambacho Wakenya wanataka kula, nitawapa,” aliambia Obinna na kufichua zaidi kuwa yeye haoni kimapenzi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved