logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Otile Brown -Baraka zetu huenda zikapitia kwa adui zetu

Mumekosa busara na unynyekevu  ndio maana mnadhani mungu aliwasahau

image
na

Makala29 September 2023 - 08:20

Muhtasari


•Mungu alitubariki zamani ila tunazipitaga njiani kila siku mana tunaedeshwa na wivu chuki na majigambo.

•Baraka zinakuja kwa njia tofauti,baraka zetu huenda zikapatikana ata kwa adui ila tunapokosa busara na unyenyekevu tutazindi kudhania kua mungu alitusahau

Mwimbaji Otile brown amewaandikia ujumbe wafuasi wake kwenye  Instargam akiwataka siku zote wazidi kuomba na kufanya mema ila wasidhani mungu amewasahau.

Kupitia ukurasa wake Otile amefichua jambo ambalo amesema kwamba watu wengi wana wivu na majigambo jambo ambalo huwafanya kupitwa na baraka zao kila wakati Otile akifichua haya kwa watu wote wanaomuunga mkono katika sanaa yake ya muziki.

 

"Mungu alishatubariki zamani ila tunazipitaga njiani kila siku mana tunaedeshwa na wivu chuki na majigambo".....Mwimbaji huyu aliendelea na ujumbe wake akisimulia zaidi alihomaanisha kwa wafuasi wake.

"Ninacho maanisha ni kwamba wakati mwingine yule unayetaka sana kumshusha huenda yeye ndio njia pekee ya mafanikio yako ". alisema mwimbaji huyu.

Otile brown kwa kumalinzia ujumbe wake aliweza kufafanua kuwepo kwa baraka za mungu katika maisha ya mwanadamu.

"Baraka zinakuja kwa njia tofauti,baraka zetu huenda zikapatikana ata kwa adui ila tunapokosa busara na unyenyekevu tutazindi kudhania kua mungu alitusahau ,wakati wote mafanikio yanaanza akilini ".Otile alisema

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved