logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Aslay asimulia kilichomgusa kuwapa wanawake Kanga siku ya maadhimisho ya miaka 10 ya mziki

Nawaheshimu sana wanawake ndipo niliamua kuwapa kanga kwa heshima ya mamangu aliyetangulia

image
na

Habari03 October 2023 - 12:41

Muhtasari


•Tulishirikiana pamoja na timu yangu kwenye siku yangu ya kusherekea miaka kumi kwenye muziki tuwape wanawake kanga ili kukumbuka mamangu na kumpa heshima yangu  ndipo niliamua kuwapa kanga wanawake

Aslay

Msanii  maarufu  nchini Tanzania wa nyimbo za Bongo Aslay, jina lake kamili Aslay Isihaka Nassoro, siku chache baada ya kuaandaa sherehe kubwa ya kuadhimisha miaka kumi kwenye muziki ametangaza kwa nini aliamua kuwapa wanawake zawadi.

Licha ya kuwa mamake mzazi alifariki akiwa mdogo sana wakati alipokuwa anachipuka kwenye  muziki Aslay alisimulia kuwanza sana jambo hilo akikumbuka upendo wa mama na jinsi alivyokuwa hodari kwa kuzitengeneza kanga.

 "Niliamua kuleta kubukumbu ya mama kwa karibu nami jinsi mama alivyopenda kanga nilipatwa na wazo na kushirikiana pamoja na timu yangu katika siku yangu ya kusherekea miaka kumi kwenye muziki tuwape wanawake kanga ili kukumbuka mamangu na kumpa heshima yangu  ndipo niliamua kuwapa kanga wanawake kwa ".Alisema aslay.

Aslay alisimulia jinsi alivyompenda mamake akisimulia kwamba alimjengea mamake nyumba akiwa na umri wa miaka kumi na tatu wakati nyota yake ya muziki ilichipuka.

Huku akiwa kwa mahojiano na wanahabari Msanii huyu wa Bongo alisimulia jinsi ambavyo amejitahidi huku akiwatangazia wafuasi wake kwamba yupo tayari kuwapa burudani mpya akiwa anashirikiana na timu yake.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved