Mashabiki wakanganywa na mapenzi ya hadharani ya Diamond na Zuchu

Katika kuonyesha ukaribu,Diamond alimlisha Zuchu kipande cha keki kwa kutumia mdomo wake,

Muhtasari

Wawili hawa,walionyesha vitendo vya mapenzi hadharani katika hafla ya awali ya sherehe,Iringa, Tanzania Octoba 6,kabla ya onyesho lao la pamoja la jumamosi.

Diamond na Zuchu
Diamond na Zuchu
Image: Instagram

Uvumi kuhusu hali ya  uhusiano wa Diamond  Platnumz na Zuchu ulikanushwa vikali na wasanii hao wawili,na kuwaacha mashabiki njia panda.

Wawili hawa,walionyesha vitendo vya mapenzi hadharani katika hafla ya awali ya sherehe,Iringa, Tanzania Octoba 6,kabla ya onyesho lao la pamoja la jumamosi.

Wakati wa tafrija hiyo,Diamond alimuita Zuchu kuungana naye baada ya kukata keki ya sherehe.

Katika kuonyesha ukaribu,Diamond alimlisha Zuchu kipande cha keki kwa kutumia mdomo wake,huku waliohudhuria hafla hiyo wakisherehekea kwa shangwe.

Aidha Msanii Diamond,alionekena akishika maziwa ya Zuchu hadharani jukwaani,akieleza kupitia wimbo jinsi anavyohisi zinavyomkoroga akili.

Uvumi wa hivi majuzi kuhusu uhusino wao ulichochewa wakati Zuchu alipojibu swali la shabiki kuhusu hisia zake dhidi ya msanii wa kenya Tanasha Donna,ambaye alimzawadi mamake Diamond Platnumz.

Jibu la Zuchu, "Sio mume wangu",awali liliibua taharuki ya kufanya mashabiki kuelewa kuwa wawili hao wameachana.

Hata hivyo Zuchu aliweka wazi hali ya uhusiano wake akisema kwamba alikuwa peke yake kw muda.

"Nimkuwa single kwa muda sasa, kwa hiyo yuko huru kufanya anachotaka." Alisema.

Kauli hii ilionekana kutoa maarifa kuhusu hali yake ya sasa ya uhusino,lakini haikuwazuia wawili hao kutokana na maonyesho yao ya hivi punde.

Kwa upande mwingine, Mama Dangote,hii karibuni aliwsihi mashabiki wasilinganishe yeye na Zuchu.

akizungumzia kama ameacha kumfuata Zuchu kwenye mitandao ya jamii,Mama Dangote alisema,

"Nishazoea mwanangu.Sijamua acha kufuata. Sasa nimu-unfollow kwa lipi? wambea wa Insta wsiniletee mambo ya kitoto. Siko kwenye level hizo,mambo yangu ni ya utu uzima."

Mama Dangote aliendelea kusema,na kudai kuwa watu wasij wakamgombanisha na mwnaye Zuchu.

"Wasinigombanishe na mwanagu Zuchu.Wote wanangu jamani,wasiniingize kwenye mambo yao. Wasilete migogoro kati yangu na mtoto wangu Zuchu.Wote ni watoto wangu,wema wangu,usinishirikishe kwenye mambo yao."

Mama Dangote lisema haya kama njia moja ya kuonyesha nia ya kukwepa kujihusisha na mabishano na vipindi mitandaoni.