Msanii Ed Sheeran aeleza kwa nini ameamua kujiandalia kaburi lake mwenyewe

Sheeran alisema kwamba alifanay hivyo kwa sababu ameshuhudia marafiki zake wakifa bila kuacha wosia na kuwaacha watu katika njia panda wasijue la kufanya.

Muhtasari

• Ingawa Sheeran amekuwa muwazi kuhusu huzuni yake kupitia muziki wake, yeye huzuia mwangaza wake mwingi wa faragha kuangaziwa.

Ed Sheeran
Ed Sheeran
Image: Instagram

Msanii wa muda mrefu wa kizazi kipya kutokea nchini Uingereza, Ed Sheeran ameushangaza ulimwengu baada ya kufichua kwamba amejiandalia kaburi lake mwenyewe katika boma lake.

Msanii huyo alifichua haya katika mahojiano yaliyochapishwa Jumatano wiki jana na GQ Hype ambapo alisema kwamba maandalizi ya kaburi hilo yamekamilika na sasa anasubiria kifo chake.

"Singesema ni siri," Sheeran, 32, aliiambia GQ Hype katika mahojiano yaliyochapishwa Jumatano. "Ni shimo ambalo limechimbwa ardhini na jiwe juu yake, kwa hivyo siku yoyote inapofika na mimi kufa, ninaingia humo."

Mwimbaji wa "Shape of You" alisema kuwa ni mahali ambapo anaweza kuomboleza watu katika maisha yake ambao wamekufa. Lilipokuwa likijengwa, aligundua angependa kuzikwa hapo ili binti zake, Lyra na Jupiter, ambao wanaishi na mke wake Cherry Seaborn, waweze kumkumbuka hapo.

Sheeran - ambaye pia hutumia mahali patakatifu kuandaa sherehe za harusi kwa marafiki zake - alibainisha kuwa pamoja na kanisa lenyewe, aliamua kutengeneza sehemu yake ya mwisho ya kupumzika ili watoto wake waje na kumkumbuka baada ya kifo chake.

"Watu wanafikiri ni jambo la ajabu na la kuhuzunisha sana, lakini nimekuwa na marafiki kufa bila wosia, na hakuna anayejua la kufanya."

Sheeran amepata hasara kubwa katika miaka kadhaa iliyopita. Mnamo 2021, mshauri wake, Michael Gudinski, alikufa akiwa na umri wa miaka 68.

 Mshindi wa Grammy alitoa heshima kwa Gudinski katika ibada yake ya ukumbusho huko Australia wakati huo, akiimba "Visiting Hours," wimbo wenye hisia kali alioandika kwa heshima ya rafiki yake. Mwaka uliofuata, Februari 2022, rafiki mkubwa wa Sheeran, Jamal Edwards, alikufa akiwa na umri wa miaka 31. Wiki chache baadaye, Sheeran alipoteza rafiki wa karibu na mchezaji wa kriketi Shane Wane, Jarida la US Daily limeripoti.

 

Ingawa Sheeran amekuwa muwazi kuhusu huzuni yake kupitia muziki wake, yeye huzuia mwangaza wake mwingi wa faragha kuangaziwa.

Sheeran anaishi katika shamba lake la Framlingham, U.K. -‚ ambalo inasemekana alilinunua kwa $5 milioni - na mkewe Cherry Seaborn na binti zao wawili, Lyra, 3, na Jupiter, miezi 17.