logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nimeamua kuchukulia utangazaji kwa Radio kwa uzito -Wema Sepetu

Wema Sepetu alitukumiwa jukumu la kuwa mshauri wa maswala ya mapenzi.

image
na Davis Ojiambo

Burudani26 October 2023 - 14:37

Muhtasari


  • • Muigizaji huyu amekuwa akifanya vipindi vya ushauri kwa kushirikisha waskilizaji ambao wanasimulia changamoto wazakumbana nazo huku Sepetu  akiwapa ushauri.
Muigizaji wa muda mrefu Wema Sepetu picha Instagram

Siku chache baada ya kukabidhiwa  jukumu la kuwa mtagazaji na mshauri wa vijana na wanandoa kwenye  kituo cha Radio Wema Sepetu  amesema kuwa amechukulia jukumu hilo kwa uzito.

Nimeamua kuchukulia jukumu langu la kutangaza kwa Radio kwa uzito ni kauli aliyochapisha kwenye mtandao wake wa instagram kwenye picha yake aliyokuwa ameshikilia kijiradio.

Muigizaji  huyo wa muda mrefu nchini Tanzania alikabidhiwa nafasi ya kuhudumu kama mtangazaji wa vipindi vya mapenzi vinavyohusisha vijana kwa kuwapa ushauri ufaao kwa kuwashauri.

Muigizaji huyu amekuwa akifanya vipindi vya ushauri kwa kushirikisha waskilizaji ambao wanasimulia changamoto wazakumbana nazo huku Sepetu  akiwapa ushauri.

Siku chache zilizopita kwenye mahojiano ya moja nyota huyu wa cinema za Bongo alifunguka na kusema kwamba alichagua kituo hicho kuelimisha watu wengi ambao wanapitia wakati mgumu kwenye familia zao na pia kwenye ndoa zao.

Mkuu wa kituo hicho baada ya kuhojiwa alifunguka na kusema kuwa walimchagua wema kwa kuwa alikuwa mfano mzuri kuigwa na waskilizaji kwani ni nyota mashuhuri anayetabuliwa na vizazi vingi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved