logo

NOW ON AIR

Listen in Live

(Video) Jinsi Sonko alitumia zaidi ya Sh1M kwa vileo kusherehekea birthday ya Uhuru Kenyatta

Sonko alifichua kwamba pombe hizo ni zile walikuwa wanatumia na Kenyatta kabla ya kukosana.

image
na Davis Ojiambo

Burudani30 October 2023 - 06:47

Muhtasari


  • • Kabla ya kulipia, Sonko alisimama mbele ya kamera na kumuimbia wimbo Uhuru Kenyatta wimbo wa kusherehekea siku ya kuzaliwa.
Sonko amsherehekea Uhuru Kenyatta

Unaambiwa mwenye pesa si mwenzio, mpishe apite!

Wakati Wakenya wengi wanalalamika vikali kuhusu gharama ya juu ya maisha, kwa aliyekuwa gavana wa Nairobi, Mike Sonko hizo ni hekaya tu za Abunuwasi.

Mfanyibiashara huyo kwa mara nyingize alionesha ubabe wake wa kifedha baada ya kutumia Zaidi ya shilingi milioni moja katika vileo ili tu kuadhimisha siku ya kuzaliwa ya aliyekuwa rais Uhuru Kenyatta.

Sonko katika mtandao wake wa X, awali ukifahamika kama Twitter wikendi iliyopita alipakia video akionesha jinsi aliingia katika duka moja la kuuza vileo na kuchagua pombe ainati zenye bei ghali ambapo baadae alilipia.

Kabla ya kulipia, Sonko alisimama mbele ya kamera na kumuimbia wimbo Uhuru Kenyatta wimbo wa kusherehekea siku ya kuzaliwa.

Pia katika maandishi kwenye video hiyo, Sonko alifichua kwamba Uhuru alikuwa ni rafiki wake miaka ya nyuma lakini walikuja kukosana wakati wa kung’atuliwa kwake madarakani kama gavana.

Hata hivyo, alipokuwa akimtakia Uhuru heri njema ya kufikisha miaka 62, alimwmabia kwamba amemsamehe kwa yote mabaya ambayo aliwahi mfanyia.

“Nampongeza Rais Mstaafu Uhuru Muigai Kenyatta. Mola Mwema akupe afya njema na maisha marefu unapoadhimisha miaka 62 ya kuzaliwa kwake. Nimekupa zawadi ya keki, kadi, na vinywaji bora zaidi kama ishara ya kukosa siku za furaha tulizozoea kutumia pamoja kabla na baada ya kuwa rais. Heri ya siku yako ya kuzaliwa, kaka yangu, na mwaka wako wa ziada ukuletee furaha,” alisema.

“Mungu anisamehe kwa matusi, maneno yasiyofaa, na chochote nilichosema ili kukuchochea ulipize kisasi. Pia nimekusamehe kwa makosa na mateso yote. Uishi muda mrefu. Mungu akubariki wewe na familia yako,” aliongeza.

Mhudumu wa duka hilo la vileo alifichua kwamba Sonko alinunua pombe yenye thamani ya shilingi milioni moja na elfu 29.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved