logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mulamwah asimulia kilichomfanya kujenga chumba cha kifahari kijijini

Millioni mbili ndio zimebaki kukamilisha nyumba  yangu asema Mulamwah

image
na

Yanayojiri02 November 2023 - 07:53

Muhtasari


•Mimi ni kioo cha jamii ,familia mingi kwenye ukoo wetu zinanitegemea ndio maana nikafanya juhudi kujenga mjengo mkubwa kwa ajili yao

Mchekeshaji mashuhuri wa Kenya David Oyando almaarufu Kendrick Mulamwah amefunguka na kusimulia kilichomfanya awe na maono ya kujenga Nyumba ya kifahari kijijini , ambayo amesema imegharimu mamilioni ya pesa.

"Maoni ya kujenga  kijijini nilitaka kufuata mfano wa babangu nikiwa mchanga  watoto wa wajomba wangu walifanikisha masomo yao kwa kuishi kwetu kwa maana babangu aliwapa makazi kwa kuwa na nyumba kubwa,"alisema.

Mulamwah alisimulia zaidi kuwa kujenga nyumba yake ni kwa ajili ya kusaidia wakiwemo ndugu,dada na amu zake wakati wanapohitaji huduma za makazi kwa maana anafahamu kule alikotoka na jamii inavyomtegemea.

Mtumbuizaji huyo mwenye umri wa miaka 30 ambaye pia ni muuguzi kwenye mahojiano alisimulia kukekwa na matusi ya wabea wakimtaja kuekeza kijijini kwa mjengo wa mamilioni ambayo angeekeza mjini kwa faida ya maisha yajayo.

"Nimepitia mengi kwenye mitandao ila kwangu nyumba yangu ndio faranja yangu wakati itakamilika najua itakuwa baraka kwa jamii yangu.

Mulamwah alisema kuwa nyumba hiyo imebakisha kiasi cha millioni  mbili ndiposa ikamilike huku akisema kuwa mipango ya kukamilisha inaendelea.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved