Meneja wa Harmonize azugumuza baada ya bosi wake kusema kalaghaiwa billioni 7

Kesi ya Harmonize ya kulaghaiwa pesa iko Mahakamani Meneja asema

Muhtasari

•Meneja huyu aliyejitabulisha kwa jina Ding'ano amesimulia kuwa ni kweli Harmonize alitapeliwa pesa hizo na kesi tayari inaendelea Mahakamani

Image: HARMONIZE

Menaja wa staa wa Bongo amejitokeza na kunzugumzia  swala la  Bosi wake kudai kuibiwa shilingi billioni saba alizowekeza hili kufungua vituo vya habari.

Kupitia mahojiano ya Moja ya moja meneja wa Harmonize amejibu madai kwenye mitandao kuwa Utajiri wa msanii Harmonize haufiki billioni saba.

Meneja huyo kwa jina Ding'ano amesimulia kuwa ni kweli Harmonize alitapeliwa pesa hizo na kesi tayari inaendelea Mahakamani.

"Harmonize ni tajari mno  mfumo  wake wa kupata  hela ni wajuu sana wengi wanakana hilo wakisema Harmonize hanauwezo wa kumiliki  billioni saba ila Harmonize ni tajiri wa zaidi ya billioni saba,"alisema.

Meneja alifunguka na kusema kwamba utajiri wa Harmonize ni wa juu akizungumzia magari ya thamani aina ta Range Rover na kumiliki magari saba aina ya V8.

Staa  huyu wa  bongo Harmonize  alisimulia  hayo wakati alipokuwa nchini Kenya mwishoni mwa wiki. Hramonise alisema alikuwa ametenga kaiasi fulani cha pesa kwa lengo la kufungua vituo vya habari ya lebo ya konde.

Ni  Siku  tu chache baada msanii Diamond Platnumz kukiri kutapeliwa shilingi billioni nne za Tanzania alizoekeza kununua ndege ya kibnafsi.

Staa huyo wa Bongofleva, amekiri alipoteza pesa hizo alizokuwa amepangia kufungua nazo nyumba ya habari ya lebo ya konde.