logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wahu azugumzia safari yake kama mlezi wa watoto watatu

Wahu aliongeza kuwa cha muhimu katika ndoa ni kuwa na upendo kwa watoto na familia nzima.

image
na

Habari10 November 2023 - 09:38

Muhtasari


•Nina mtoto wa miaka kumi na saba,wa pili miaka kumi na kitinda mimba wangu ni mwaka mmoja na mwezi ,

• Watoto hao wote kila mmoja  ana mahitaji yake maalum, huwalea ili wawe na maisha mazuri kuliko yangu,'alisema.

Nameless na Wahu

Mwanamuziki maarufu wa Kenya Wahu Kagwi amemshukuru Mungu kwa baraka, kumfanya kuwa mama mlezi wa watoto watatu na ndoa ya miaka kumi na minane

"Wengi huniuliza safari ya kulea iko aje?,ila kwangu ni neema kubwa kuwa ndani ya ndoa kwa miaka 18, kuwa mama wa watoto watatu mlezi ya miaka 17 ni jambo ambalo mimi hujivunia na kushukuru Mungu kwa upendo  kwa familia yangu," alisema Wahu.

Mwanamuziki huyo alisimulia zaidi, kuwa mama wa watoto watatu ni jambo ambalo humfurahisha. Alisema yeye wanawe ni marafiki mno jambo ambalo limemsaidia sana kujua changamoto wanazopitia.  

"Nina mtoto wa miaka kumi na saba,wa pili miaka kumi na kitinda mimba wangu ni mwaka mmoja na mwezi ,watoto hao wote kila mmoja  ana mahitaji yake maalum, huwalea ili wawe na maisha mazuri kuliko yangu,'alisema.

Wahu aliongeza kuwa cha muhimu katika ndoa ni kuwa na upendo kwa watoto na familia nzima.

 

Hayo yanajiri siku chache baada ya The Mathenges, kama wanavyojiita kuadhimisha miaka 18 pamoja kwa safari ya ndoa.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved