logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Lynne ambwagia sifa kemkem mpenzi wake Eric Omondi

"Haya mapenzi sitatoka kamwe ndio yenye upendo mwingi na furaha," alisema Lynne.

image
na

Yanayojiri10 November 2023 - 11:16

Muhtasari


•Lynne alikiri upendo mkubwa kwa mpenzi wake na kubainisha kuwa yeye ndiye mwanamke mwenye bahati sana  duniani kwa kuwa kwenye mahusiano na Eric Omondi.

Lynne Njihia , mke wa mchekeshaji Eric Omondi amelimbikizia sifa tele kwa jinsi anavyotumikia familia yake kwa upendo na furaha wakati wanapomlea mtoto wao mchanga wa miezi mitatu,wayempa jina Kaylar.

Kwenye mahojiano ya moja kwa moja, Lynne alikiri upendo mkubwa kwa mpenzi wake na kubainisha kuwa yeye ndiye mwanamke mwenye bahati sana  duniani kwa kuwa kwenye mahusiano na Eric Omondi.

"Haya mapenzi sitatoka kamwe ndio yenye upendo mwingi na furaha," alisema Lynne.

"Najivunia sana kuwa mwanamke mwenye bahati sana  duniani napedwa sana, japo kuwa Eric amependa mtoto wake Kaylar kuniliko, hiyo ndio furaha ya maisha yangu,"alisema.

Aidha, alifichua maelezo kuhusu safari yao nje ya nchi ambapo alisimulia kuwa wapanga kumtembeza mtoto wao mchanga kwani walimchukulia pasipoti akiwa na umri wa wiki mbili.

"Mtoto wetu anafaa kutembea kwani ni mtoto wa Rais wa vishekesho 'malkia Kaylar', kila stakabadhi ya kusafiri zimo, tupanga kumtembeza mataifa ya nje,"alisema.

Kwenye mahojiano hayo, Lynne alisema kuwa wameongeza pesa za kuona mtoto wao kutoka kwa millioni hamsini hadi sabini.

"Venye Rais Ruto ameongeza bei ya bidhaa nchini, pia sisi tumeogeza bei kwa yeyote yule anataka kumuona mtoto wetu hadi milioni sabini,"alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved