logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Diamond kukutanishwa na 'role model' wake wa mavazi, Asake kwenye jukwaa moja

Shoo hiyo itafanyika kuanzia tarehe 26 Juni mpaka tarehe 28.

image
na Radio Jambo

Habari15 November 2023 - 07:37

Muhtasari


• Tangazo la wawili hao kujumuishwa kwenye tamasha hilo lilizua minong’ono mingi kutoka kwa mashabiki wa Bongo Fleva.

Asake na Diamond

Waandaaji wa tamasha la Afro Nations wametoa orodha rasmi ya wasanii wa Kiafrika ambao watatumbuiza kwenye tamasha hilo mwezi Juni mwaka ujao nchini Ureno.

Na katika orodha hiyo, kwa mara ya kwanza msanii Diamond Platnumz atakutanishwa na Asake, msanii anayekuja kwa kasi Zaidi kutoka nchini Nigeria ambaye kwa mara nyingi Diamond ametuhumiwa ku,uiga katika mavazi, mitindo ya nywele lakini pia hadi kutembea na vitu vingine.

Kwa upande wa wapenzi wa muziki wa Bongo Fleva, mashabiki wengi wamekuwa wakisema kwamba msanii Diamond anamuiga sana Asake katika vitu vingi tu licha ya kwamba Asake hana muda mrefu kwenye tasnia na yeye Diamond amekuwa karibia miaka 15 kwenye muziki sasa.

Sasa tangazo la wawili hao kujumuishwa kwenye tamasha hilo lilizua minong’ono mingi kutoka kwa mashabiki wa Bongo Fleva ambao wanahisi kwamba hii itakuwa mara ya kwanza kuona nani mkali wao kwenye jukwaa.

Shoo hiyo itafanyika kuanzia tarehe 26 Juni mpaka tarehe 28 na baadhi ya majina makubwa ambao watatumbuiza ni pamoja na Rema, Asake, Ninho, Omah Lay, Mr Falvour, Diamond Platnumz, Tyla, Seyi Vibez, The Compozers, Odumodublvck miongoni mwa wengine.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved