logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kwa mara ya kwanza Diamond Platnumz amerudia vazi alilolivaa mara ya mwisho 2019

Wewe hurudia nguo baada ya kipindi kipi?

image
na Davis Ojiambo

Burudani16 November 2023 - 12:27

Muhtasari


  • • Kupitia instastory yake, Diamond mwenyewe aliwafungua macho na wigo wa fikira mashabiki wake.
Diamond Platnumz

Kwa mara ya kwanza tangu mwezi Februari mwaka 2019, msanii Diamond Platnumz amerudia nguo ambayo aliivaa mara ya mwisho mwaka huo kipindi wanafanya video ya Tetema – kolabo aliyoshirikishwa na Rayvanny.

Msanii huyo hivi majuzi ameachia kolabo ya Commando, akishirikishwa na msanii G Nako na katika moja ya scene, alionekana na koti rangi inakaribia kuwa waridi.

Mashabiki wengi hawakuweza kubaini kuwa koti hilo ndilo lile alilovaa wakati wanafanya video ya Tetema 2019.

Kupitia instastory yake, Diamond mwenyewe aliwafungua macho na wigo wa fikira mashabiki wake kwa kufichua kwamba ndilo lile lile vazi ambalo amelitunza kwa muda huo ambao unagonga Zaidi ya miaka minne na ushee.

Diamond alijipa hongera kwa utunzaji wa kipekee akisema kwamba si watu wengi ambao wanaweza onyesha mavazi yao ya miaka 4 iliyopita yakiwa katika hali shwari utadhani yametoka sokoni juzi.

“Nikuibie siri tu kwamba koti nililolivaa kwenye Komando ndilo koti lile lile nililolivaa zamani kwenye video ya Tetema. Hii inaitwa utunzaji na kuheshimu mali, kiufupi kutotumia hela ovyo,” Diamond alisema.

Ni adimu kwa wasanii na mastaa wengi kurudia nguo, Diamond akiwa mmoja wao ambaye huonekana na vazi moja kwa mara moja tu bila kulirudia.

Wewe hurudia nguo baada ya kipindi kipi?


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved