logo

NOW ON AIR

Listen in Live

DJ Pierra Makena afichua maswali magumu anayoulizwa na bintiye kuhusu babake

Makena alifichua kwamba wakati mwingine mtoto anamuuliza baba yuko wapi.

image
na Radio Jambo

Habari17 November 2023 - 07:57

Muhtasari


• “Naamini wakati atakuwa mtu mzima, atajua dunia ikoje, na natumai hatokuja kulifikiria kwa njia hasi.”

DJ Pierra Makena.

DJ Pierra Makena amefunguka kwamba kumlea mtoto bila uwepo wa baba katika maisha yake kunakuja na changamoto si haba.

Akizungumza katika mahojiano na Mungai Eve, Makena alifichua kuwa binti yake wa miaka 7 ambaye hajawahi muonesha baba yake tangu kuzaliwa.

Alisema kwamba baba mwanawe alimtoroka akiwa na mimba ya wiki mbili na kufunga ndoa miezi mitano baadae na hiyo ndio mara ya mwisho walionana na yeye wakiwa katika mahusiano.

Makena alisema kwamba haijakuwa rahisi kumlea binti kwa miaka 7 pasi na kuwepo kwa baba na akasema kwamba mtoto huyo humkabili na maswali magumu sana.

Makena alifichua kwamba wakati mwingine mtoto anamuuliza baba yuko wapi na inambidi kuibua majibu ya kughushi ilmradi tu kumtuliza.

“Wakati anauliza maswali kama hayo kuhusu babake, ana wazo kwa mbali kuhusu babake lakini maswali ambayo anauliza ni ‘lakini niliwahi kumuona, wa hiyo ako wapi?’ lakini wakati anauliza huwa namjibu unajua ‘babako alisafiri’ au ‘ako tu bize atakuja mkutane ako mbali kikazi’… huwa najaribu kukwepa masuala kama hayo lakini pia huwa najaribu kumhakikishia kwamba ‘unajua babako anakupenda’ ili tu kuhakikisha kwamba haimuathiri kwa njia hasi,” alisema.

Makena alisema kwamba huwa inamlazimu kumdanganya mtoto kwamba babake anampenda japo kuwa wakati mwingine si kweli lakini ni kwa ajili tu ya kumhakikishia mtoto upendo kutoka kwa mdomo wake.

Lakini pia alisema kwamba hatolificha hilo kwa muda wote kwani mtoto atakua na atajua jinsi dunia ilivyo na kujua kutenganisha maji na mafuta.

“Naamini wakati atakuwa mtu mzima, atajua dunia ikoje, na natumai hatokuja kulifikiria kwa njia hasi.”


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved