logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwili wa msanii aliyekufa wasimamishwa wima ili mashabiki waupigie kwaheri (video)

Maiti hiyo pia ilivalishwa kamili kama mtu aliye hai kuanzia nyayo hadi utosi.

image
na Radio Jambo

Habari01 December 2023 - 10:53

Muhtasari


• 2pm alikutana na kifo chake katika ajali mbaya iliyotokea Ijumaa, Novemba 17, huko Wassa Akropong, Mkoa wa Magharibi wa Ghana.

Mwili wa 2PM

Kwa mara nyingine tena raia wa Ghana wamezua gumzo katika mitandao ya kijamii kuhusu utamaduni wa kuaga marehemu.

Kisa cha kushangaza ambacho kimezua mjadala pevu katika mitandao ya kijamii ni baada ya mwili wa msanii mmoja aliyefariki kwa ajali wiki iliyopita ulivyoagwa na umma na mashabiki wake.

Katika picha na video ambazo zimeenezwa kwenye mitandao ya kijamii, rapa huyo kwa jina 2pm alitolewa mochwari na kufikishwa nyumbani kwake lakini kabla ya maziko, mashabiki wake wakataka kumupa buriani kwa kuutazama mwili wake kwa mara ya mwisho.

Kwa kawaida aktika jamii nyingi, mwili hutazawa ukiwa umelalishwa ndani ya jeneza, lakini nchini Ghana hali ni tofauti; mwili wa kijana huyo uliondolewa mazima ndani ya jeneza na kuegemezwa kwa kusimamishwa wima huku watu wkaipita na kuutazama utadhani ni kinyago kilichokuwa kimevalishwa nguo.

2pm alikutana na kifo chake katika ajali mbaya iliyotokea Ijumaa, Novemba 17, huko Wassa Akropong, Mkoa wa Magharibi wa Ghana.

Maiti yake ilikuwa imesimamishwa ndani ya kijumba cha glasi ukiwa umevalishwa kofia, saa, mavazi aliyopenda kuvalia, cheni kifuani lakini pia fimbo mkononi, kwa mbali ungedhani ni kinyago cha kuuza nguo kumbe ni maiti.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved