• Hivi majuzi, muigizaji huyo aligonga vichwa vya habari baada ya kupakia video akila msosi wa ajabu wakati wa ziara yake nchini Benin.
• Lupita katika video hiyo alikuwa akila kwa mara ya kwanza nyama ya nyoka aina ya Viper.
Muigizaji wa Kenya anayeishi Mexico, Lupita Nyong’o ametoa orodha ya nyimbo 10 bora ambazo angependelea kuzisikiliza Zaidi mwaka wa 2024.
Kupitia Instagram yake, Lupita Nyong’o alipakia orodha ya ngoma 10 pendwa kwa mwaka 2024 na kwa bahati nzuri kati ya ngoma hizo 10, mbili ni za kutoka Afrika Mashariki.
Mshindi huyo wa tuzo za Oscar mwaka 2014 aliorodhesha ngoma ya Kuna Kuna ya msanii Vic West akiwashirikisha wasanii wa Gengetone kama Brandy Maina, Fathermoh, Thee Exit band na Savara kama wimbo wa Kikenya ambao unampunga sana na angependa kuusikiliza tena mwaka 2024.
Pia katika orodha hiyo alitaja wimbo wa Enjoy wake Juma Jux akimshirikisha Diamond Platnumz kutoka Tanzania, ukiwa katika nafasi ya 7.
Nyimbo nyingine ambazo Lupita aliorodhesha ni pamoja na;
This Year wa Emily King
Good Morning wa PJ Morton
It’s So Easy wa Margo & Mac
Deggi Gui wa Cheikh Lo
Next to Normal wa Lucius
Nueva Vida wa Peso Pluma
By Design [Evel Knievel] na Jacob Banks
Doing my Best na Tank and The Bangas
Hivi majuzi, muigizaji huyo aligonga vichwa vya habari baada ya kupakia video akila msosi wa ajabu wakati wa ziara yake nchini Benin.
Lupita katika video hiyo alikuwa akila kwa mara ya kwanza nyama ya nyoka aina ya Viper.
Baada ya kuonja kwa woga mwingi, muigizaji huyo alionekana kufurahia akisema kwamba nyama ya nyoka kwa asilimia kubwa ladha yake inawiana na ya kuku.