Ukifurahisha mwanamke utajua wanawake wanapenda mapenzi kuliko wanaume - Dacha

“That's true halafu ukuwe na pesa kidogo ya kuspice it baas” Andy Eugene alisema.

Muhtasari

• Dacha ambaye hajawahi hisi kunyanyapaliwa kutokana na umbile lake kubwa aghalabu hujiita mashine kubwa kwa maana ya kujikubali na maumbile yake.

SANDRA DACHA
SANDRA DACHA
Image: Facebook

Muigizai Sandra Dacha ameibuka na ushauri mwingine kwa wanaume ambao wanashinda kulalamika kwamba wanawake wengi wanawapenda kwa ajili ya wanachowapa wala si kwa ajili ya mapenzi.

Dacha kupitia ukurasa wake wa Facebook anashauri kwamba mwanamume yeyote akitaka kujua kwamba mwanamke anapenda kushiriki mapenzi na mwanamume anayempenda basi mwanzo hakikisha mwanamke huyo ametulia na kustarehe.

Mwigizaji huyo alisema kwamba pindi mwanamke anapokuwa ametulia na kufuraia, hapo ndipo ukweli wake utajidhihirisha kwamba wanawake wanapenda mapenzi Zaidi hata ya jinsi wanavyoweza kuwapenda wanaume kwa vitu vyao.

“Mwanamke anapokuwa na raha na wewe ndipo utajua kuwa wanawake wanapenda zeks [ngono] kuliko wanaume,” Dacha alisema.

Dacha ambaye hajawahi hisi kunyanyapaliwa kutokana na umbile lake kubwa aghalabu hujiita mashine kubwa kwa maana ya kujikubali na maumbile yake.

Katika upande wa kutoa maoni, mashabiki wake waligawanyika pande mbili, warembo wengi wakionekana kukubaliana na yeye huku wanaume wakibisha kwamba hakuna litakaloshindikana kwao.

“Hakuna mkate mgumu mbele ya chai,” Ben Ule msee Nyabera.

“Uko na busara kibao,” Stella Charisma alimwambia.

“And where is the lie?” Sharon Akinyi Abuto.

“Hi mwaka umeamua kuachilia ukweli yote” Muranga’a County Politics.

“That's true halafu ukuwe na pesa kidogo ya kuspice it baas” Andy Eugene.