logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Sababu ya Babu Owino kuchukua breki katika masomo yake ya shahada ya 3 ya uzamili

Katika chapisho hilo, Owino alikuwa ameketi mezani na mbele yako kukiwa na rundo la vitabu ainati.

image
na Davis Ojiambo

Burudani30 January 2024 - 11:26

Muhtasari


  • • “Ninapiga kurasa hizi kwa nguvu katika mpango wangu wa kuhakikisha siwaonei huruma watahini wangu,” Owino alisema.
BABU OWINO.

Mbunge wa Embakasi Msshariki Babu Owino amefichua kwamba katika kipindi cha mwezi mmoja uliopita, amekuwa akijishughulisha na kubukua vitabu akifanya maandalizi kwa ajili ya mtihani wake wa kufuzu shahada ya tatu ya uzamili.

Mbunge huyo sasa amesema kwamba atachukua mapumziko ya muda kukaa mbali na vitabu kwa muda kwa ajili ya kujipa muda ili kushiriki katika mchakato wa chama chake cha ODM wa kuandikisha wanachama Zaidi jijini Nairobi.

“Kwa muda wa mwezi mmoja uliopita, nimekuwa nikila vitabu kama viazi vikuu nikijiandaa kwa mitihani yangu ya Shahada ya 3 ya Uzamili. Lakini nitapumzika kwa muda mfupi kwa shughuli ya kuajiri ODM jijini Nairobi kabla ya kuanza tena mashambulizi yangu ya kitaaluma. Mungu anibariki,” Babu alisema.

 Mbunge huyo msomi ambaye ametajwa kuwa huenda atajitosa katika kinyang’anyiro cha ugavana Nairobi uchaguzi mkuu wa 2027 alizidi kujitapa akisema kwamba kwa kawaida yeye huwa haonei vitabu huruma pindi anapoketi kuvibukua.

“Ninapiga kurasa hizi kwa nguvu katika mpango wangu wa kuhakikisha siwaonei huruma watahini wangu,” Owino alisema.

Katika chapisho hilo, Owino alikuwa ameketi mezani na mbele yako kukiwa na rundo la vitabu ainati.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved