logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kodi yangu ya nyumba kwa mwezi ni shilingi 350K - Amber Ray

“Weeeeh si 300k ni 350k tafadhali, mbona mnatoa hiyo 50k?” Ray aliuliza.

image
na Radio Jambo

Habari02 February 2024 - 05:15

Muhtasari


• Mama wa watoto wawili alionyesha nyumba yake mpya, kamili na lifti.

•Katika video hiyo, alishuka kutoka kwenye lifti, ambayo ilifungua moja kwa moja kwenye sebule yake, akitembea hadi kwenye ukumbi akiwa na glasi ya mvinyo mkononi.

Amber Ray na Kennedy Rapudo

Mwanasosholaiti Amber Ray amefichua kwamba kwa kila mwezi, yeye na mpenzi wake Kennedy Rapudo hulipa kodi ya nyumba Zaidi ya shilingi za Kenya laki tatu.

Ray alikuwa anamjibu kwa kumkosoa mwanablogu mmoja ambaye alikuwa makini kugundua kwamba Amber Ray na mpenzi wake wamebadilisha mazingira ya nyumba walimokuwa wakiishi hapo awali.

Mwanablogu huyo alipakia video ya Amber Ray akiwa anashuka katika ngazi za nyumba hiyo na kufichua kwa jicho la udadisi kwamba huenda Amber Ray na Kennedy Rapudo walihama kamazi yao ambapo walikuwa wakilipa kodi ya laki mbini na nusu kwa mwezi.

Alisema kwamba wawili hao walihamia nyumba nyingine ya kifahari yenye vyumba vitano ambayo kodi yake ni shilingi laki tatu.

“Inaonekana ni kama Amber Ray na babydaddy wake walihama katika makazi yao ya kifahari yenye kodi ya kila mwezi 250k na kuhamia nyumba nyingine ya kifahari yenye vyumba 5 ambayo kodi ni 300k,” Mwanablogu huyo alidadisi.

Hata hivyo, Amber Ray alifika kwenye chapisho hilo na kumkosoa mwanablogu huyo kwamba si 300k bali ni 350k, akimtanga kuzingatia hiyo elfu 50 ya juu.

“Weeeeh si 300k ni 350k tafadhali, mbona mnatoa hiyo 50k?” Ray aliuliza.

Juzi kati, sosholaiti huyo mwenye maisha laini na mfanyabiashara mume wake, Rapudo  waliwafurahisha mashabiki wao kwa kushiriki video ya makazi yake mapya ya kifahari.

Mama wa watoto wawili alionyesha nyumba yake mpya, kamili na lifti. Katika video hiyo, alishuka kutoka kwenye lifti, ambayo ilifungua moja kwa moja kwenye sebule yake, akitembea hadi kwenye ukumbi akiwa na glasi ya mvinyo mkononi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved