logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Muigizaji Wolper aapa kuzaa hadi watoto 6 ili kuwakomesha waliomdhihaki kuwa ni tasa

Wolper alisema tumbo lake limeongezeka kutokana na kuwa na stress.

image
na Davis Ojiambo

Burudani20 February 2024 - 06:24

Muhtasari


  • • “Nina stress zangu tu yaani hapa ni kula na kusimamia mambo yangu, sina mimba." alisema.
Jackline Wolper na wanawe

Muigizaji mkongwe wa filamu za Bongo ambaye pia ni mjasiriamali Jackline Wolper ameweka wazi kwamba kwa sasa hana mimba nyingine baada ya watu kuanza kushuku ukubwa wa tumbo lake.

Mama huyo wa watoto wawili alisema japo kwa sasa hana mimba, lakini hata akipata mimba ataificha hadi watu waje kushutkia siku ya mwisho kuwa ana mtoto, kama ambavyo amefanya awali kwa watoto wake wawili.

“Yaani mna haki kuniambia nina mimba jamani, eeh… kitambi kimeongezeka balaa, lakini sina mimba, sina! Washenzi wakubwa nyie. Na nikiwa nayo naficha vile vile kama kawaida. Uchawi tu ‘una mimba una mimba’” alisema huku akilipiga makofi tumbo lake.

Wolper alifichua kwamba anataka kuja kuwakomesha wote waliomdhihaki kuwa yeye ni tasa ambaye hawezi kubeba ujauzito, akisema kwamba kama njia moja ya kuwakomesha na kuwaziba midomo, atahakikisha amezaa hadi watoto sita.

“Nina stress zangu tu yaani hapa ni kula na kusimamia mambo yangu, sina mimba. Japokuwa ninataka nikimalizana na mambo yangu nizae kweli kweli. Si mliniita mgumba nyine, nitawapa shoo bado, napia hadi sita ndio napumzika,” aliongeza.

Mama P, kama anavyojiita alifunga harusi miaka miwili iliyopita na mpenzi wake Rich Mitindo na wamekuwa wakiyaweka maisha yao ya ndoa mbali na mitandao ya kijamii.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved