Otile Brown atumbuiza waombolezaji na kibao cha 'One call' kwenye mazishi ya Chira

Wimbo huo kwa sasa una maoni zaidi ya milioni nne kwenye YouTube.

Muhtasari
  • Chira atazikwa leo(Jumanne) nyumbani kwa familia yake huko Gathanje, kijiji cha Ingitei, Githunguri kaunti ya Kiambu.
amemuomboleza Brian Chira
Otile Brown amemuomboleza Brian Chira
Image: INSTAGRAM

Mwanamuziki Otile Brown Jumanne aliimba kibao chake cha  'One Call' kwenye mazishi ya TikToker Brian Chira,kibao ambacho kinaaminika kuwa Chira alikipenda.

Alipanda jukwaani na kuimba wimbo huo huku waombolezaji wakiimba pamoja naye kwenye wimbo huo.

"One call away Call me if you need me. Shujaa wako. I'm only one call away," waliimba.

Hapo awali mwimbaji huyo alijitolea kutumbuiza wimbo huo kwenye mazishi ya Chira akikiri Chira aliupenda wimbo huo.

"Ningependa kutumbuiza wimbo huo wakati wa maziko na kunisaidia kuifanya iwe ya kumbukumbu kwake ikiwezekana," alisema na zaidi kuwataka waliohudhuria maziko hayo kujifunza mashairi ya wimbo huo.

Wimbo huo ulikuwa wimbo alioupenda zaidi Chira na mwimbaji huyo alikiri kuwa kifo chake kiliwafanya Wakenya kumiminika katika chaneli yake ya YouTube ili kutiririsha wimbo huo.

"Kile Chira anachofanya kwenye #OneCall ni cha ajabu. Nuru yake ni angavu na upendo unasikika. Rest well King," Otile Brown alikuwa ameandika hapo awali kwenye mitandao ya kijamii,huku akimuomboleza.

Wimbo huo kwa sasa una maoni zaidi ya milioni nne kwenye YouTube.

Brian Chira aliaga dunia Jumamosi, Machi 16 baada ya kugongwa na lori lililokuwa likienda kasi.

Chira atazikwa leo(Jumanne) nyumbani kwa familia yake huko Gathanje, kijiji cha Ingitei, Githunguri kaunti ya Kiambu.

“Ni kwa mioyo mizito na kukubali mapenzi ya Mungu kwamba tunatangaza kufariki kwa ghafla kwa mpendwa wetu Brian Chira Wambui, ambaye alienda kuwa na Bwana mnamo Machi 16 huko Kiambu,” familia hiyo ilitangaza.

"Mikononi mwa Mungu, unapumzika, ndani ya mioyo yetu unaishi milele." Warumi 8:18 - Lakini