logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Wivu tu ndio imewajaa...' Babushka awajibu wanaokosoa kazi zake za hisani

Babushka amewajibu wale wanokosoa kazi zake za hisani kwa madai ya kupata umaarufu

image
na Radio Jambo

Burudani24 May 2024 - 09:04

Muhtasari


•Babushka amekuwa mstari wa mbele kutoa misaada huku baadhi wakisema anafanya hivyo ili kupata umaarufu kwenye mitandao ya kijamii. 

BABUSHKA

Mtayarishaji wa maudhui ya kidijitali Kennedy Matiso Rioba maarufu kama Babushka amejibu wale wanaomkosoa kuhusu kazi zake za uhisani.

Kupitia ukurasa wake rasmi wa Instagram, Babushka ambaye amekuwa mstari wa mbele kutoa msaada kwa wahitaji alisema kwamba hataacha kazi yake ya uhisani kwa sababu ya kukosolewa baada ya kushutumiwa kwa kutumia kazi yake ya hisani kupata umaarufu kwenye mitandao ya kijamii.

"Wivu tu ndio imewajaa, tutasonga mbele bila kujali," Mtayarishaji wa maudhui huyo alisema.

 Kennedy Matiso aliyeyusha mioyo ya mashabiki wake baada ya kufichua mipango yake ya kujenga daraja katika Kaunti ya Nairobi, Kasarani Machi, 2024 kupitia wakfu ya uhisani iliyopewa jina Babushka Foundation.

Huu ni mradi wake wa kwanza chini ya taasisi yake ya uhisani mbali na kazi yake ya hisani, Babushka anajulikana sana kwa kuburudisha watumiaji wa mtandao kupitia miondoko yake ya ngoma.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved