Willis Raburu anafunguka kuhusu kufiwa na bintiye

" Kama baba, nilihisi kama nimeibiwa nafasi hiyo. Nilijiuliza, mimi bado ni baba?"

Muhtasari

•Willis Raburu alishiriki mipango aliyokuwa nayo kwa bintiye na mke wa zamani Marya Prude kabla ya kumpoteza wakati wa kujifungua.

•Mwanahabari huyo alieleza kuwa alijaribu kumwita baada ya kuzaliwa, lakini hakujibu wala kukohoa, hivyo kumpeleka katika msimu wa huzuni.

•Aliongeza kuwa kuna nyakati bado anamkumbuka anapoona picha zake kwa sababu alifanana naye.

Willis Raburu katika studio za Radio Jambo
Image: RADIO JAMBO

Mwanahabari maarufu Willis Raburu amefunguka kuhusu marehemu bintiye Adana, ambaye alikuwa na mke wa zamani Marya Prude.

Raburu, katika mahojiano na Parents Magazine, alishiriki kwamba bado anamfikiria marehemu binti yake kwa sababu ya uwekezaji aliokuwa ameufanya kabla ya kufa mwaka wa 2019.

Willis alisema kwamba wakati wa ujauzito wa Marya, alianza kufanya ununuzi wa vitu na kuagiza zawadi kutoka kwa wavuti ya Manchester United kwa binti yake.

Pia aliongeza kuwa alikuwepo wakati wa ziara za kliniki na kwamba alikuwa amewaza ni aina gani ya maisha anayotaka kwa binti yake.

Hata hivyo, siku ambayo mke wake wa zamani alikuwa akijifungua, Raburu alisema kwamba aliambiwa binti yake hana mapigo ya moyo.

"Nilimshika mtoto wangu. Nilimwita  mara nyingi. Hakunijibu, hakukohoa. Hakukuwa na muujiza kama nilivyotarajia. Kama baba, nilihisi kama nimeibiwa nafasi hiyo. Nilijiuliza, mimi bado ni baba?" Alisema.

Mwanahabari huyo pia alibainisha kuwa bado anapata nyakati zinazomkumbusha kuwa katika chumba cha maiti na marehemu bintiye.

Pia aliongeza kuwa baadhi ya nyimbo pia humkumbusha marehemu bintiye na kwamba mtu huwa haishiwi na huzuni.

Raburu alikumbuka kuvunjika moyo kila wakati msimu huo na akawashauri wanaume kufunguka kuhusu huzuni.