logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“Sihitaji kufanya DNA tena!” MP Kaluma aonyesha furaha bintiye kushiriki maandamano ya Gen Z

“Hapa sihitaji tena kufanya DNA, binti yangu huyu,” Peter Kaluma alisema.

image
na Davis Ojiambo

Burudani25 June 2024 - 11:32

Muhtasari


    Mbunge wa Homa Bay Mjini Peter Kaluma ameonyesha furaha yake baada ya kumshuhudia binti yake akiwa miongoni mwa vijana wengi waliojitokeza kushiriki maandamano ya kupinga kupitishwa kwa muswada tata wa fedha 2024.

    Kupitia ukurasa wake wa X, Zamani jukwaa likijulikana kama Twitter, Kaluma alipakia video ya binti yake mwenye umri wa makamo akiandamana na wenzake huku akiwa anapeperusha bendera.

    Kaluma alisema kuwa sasa amethibitisha uhalisia wa kuwa huyo ni mwanawe na hahitaji tena kufikiria kufanya DNA.

    “Hapa sihitaji tena kufanya DNA, binti yangu huyu,” Peter Kaluma alisema.

    Awali tuliripoti kwamba mbunge huyo wa Azimio alikuwa ametoa onyo kwa wanawe wote kwamba wasipojitokeza kujiunga na wenzao katika kushiriki maandamano, atatilia shaka kuwa ni wanawe na atafikiria kufanya vipimo vya DNA.

    "Mtoto wangu yeyote ambaye hataungana na watoto wengine wa Kenya mitaani Jumanne hii kupinga kutozwa ushuru kupita kiasi na ufisadi wa serikali atakabiliwa na kipimo cha DNA! Watoto wa Kenya lazima watembee pamoja ili kufaulu tulipofeli," mbunge huyo alisema.

    Hii hapa video bintiye akiandamana;


    RADIO JAMBO FREQUENCIES

    Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


    logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved