logo

NOW ON AIR

Listen in Live

‘Hatutaki, hatutajoin! - Eric Omondi asema kuhusu mazungumzo ya Rais na vijana kwenye X Space

Eric alifichua kukataliwa kwa Mswada wa Fedha uliopendekezwa ni kura ya kutokuwa na imani na utawala wa Ruto

image
na Davis Ojiambo

Burudani05 July 2024 - 10:17

Muhtasari


  • •Eric alibainisha kuwa kukataliwa kwa Mswada wa Fedha uliopendekezwa ni kura ya kutokuwa na imani na utawala wa Ruto.
  • •Eric Omondi alizidi kufichua kuwa Wakenya wamechanganyikiwa kwa muda mrefu kutokana na gharama ya juu ya maisha na kuongeza kuwa Mswada huo wenye utata ulikuwa kichochezi tu.

Mchekeshaji Eric Omondi ametoa maoni yake kuhusu mkutano wa Rais William Ruto  na Gen  Z kwenye jukwaa la X space.

Akizungumza wakati wa mahojiano Eric Omondi ambaye amekuwa mstari wa mbele kukosoa utawala wa Ruto, alisema kuwa kama vijana hawako tayari kufanya mazungumzo yoyote na rais.

Eric alibainisha kuwa kukataliwa kwa Mswada wa Fedha uliopendekezwa ni kura ya kutokuwa na imani na utawala wa Ruto.

Pia aliongezea kwamba Wabunge waliounga mkono Mswada huo wenye utata pamoja na Mkuu wa Nchi wanapaswa kujiuzulu.

“Hatutaki! Hatutajoin. Tumepangwa ya kutosha. Tunataka Ruto aende. Chochote wanasema hatukubali,” alisema.

“Suluhu ya shida ya Kenya ni ikiwa Rais Daktari Ruto, waziri wake, na wale waliovote Ndiyo watajiuzulu. Ni kura ya kutokuwa na imani.”

Eric Omondi alizidi kufichua kuwa Wakenya wamechanganyikiwa kwa muda mrefu kutokana na gharama ya juu ya maisha na kuongeza kuwa Mswada huo wenye utata ulikuwa kichochezi tu.

“Wakenya wamesema sio Mswada wa Fedha, Mswada wa Fedha tumetumia kuongea uchungu na matakwa yetu."

"Bili ya fedha ni trigger tu. Hatutaki, hatukubali, tutambandua na tutatumia sheria,” alisema

Msemaji wa Ikulu Hussein Mohamed mnamo Alhamisi, Julai 4, 2024, katika chapisho  kwenye X  alifichua kuwa Ruto atashirikiana na vijana kwenye X Space leo kuanzia 2pm -5pm.

Rais William Ruto anatazamiwa  kuwa mwenyeji wa mazungumzo yake ya kwanza ya X-Space (zamani Twitter) na vijana wa Kenya mwendo wa saa nane mchana hadi saa kumi na moja jioni leo.

Kulingana na Ikulu, baraza la mawaziri limepangwa kujiunga na majadiliano ya mtandaoni ya saa tatu. 'X Spaces', ni kipengele kinachokuruhusu kuwa na mazungumzo ya moja kwa moja ya sauti kwenye jukwaa la mitandao ya kijamii.

Wakenya wamealikwa kujiunga na mjadala wa X Space kuanzia saa nane mchana hadi saa kumi na moja jioni


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved