Vivianne asimulia suala ambalo lilimsukuma kuacha pombe

“Kuwa mchekeshaji hakukuniepusha na hilo bali niliacha kucheza nao kwani ni sawa na kucheza na moto utakuchoma tu," alisema.

Muhtasari

•Msanii huyo alifananisha ulevi kama kucheza na moto, haswa wakati mtu hawezi kujidhibiti.

•Aliendelea kuongeza jinsi anahisi mazungumzo kuhusu matumizi mabaya ya pombe daima yamegubikwa na aibu ambayo inafanya iwe vigumu kwa watu ambao wanaweza kutaka kutafuta msaada kukwepa kufanya hivyo.

Mwanamuziki Vivian

Msanii na mwandishi wa nyimbo za injili Vivianne Wambui Ndirangu almaarufu Vivian KE amefunguka kuhusu safari yake ya kuwa sobber na kilichomsukuma kuelekea kunywa pombe.

Akielezea kupitia mtandao yake ya kijamii mama wa mtoto mmoja alisimulia jinsi ulevi umekuwa tabia katika familia yake na nia yake ya kuvunja mzunguko huo.

 Hasa kwa vile alikuwa ameona jamaa wengi sana wakipoteza maisha kwa sababu ya tabia mbaya.

"Mimi ni miongoni mwa wale ambao wamekulia katika familia ambayo ulevi umeangamiza maisha ya watu wengi. Ni hali ya kawaida sana ambayo ninaamini inashughulikiwa kwa njia ya kawaida au kufichwa kwa aibu," msanii huyo aliandika kwa sehemu.

Aliendelea kuongeza jinsi anahisi mazungumzo kuhusu matumizi mabaya ya pombe daima yamegubikwa na aibu ambayo inafanya iwe vigumu kwa watu ambao wanaweza kutaka kutafuta msaada kukwepa kufanya hivyo.

“Kutokana na madhara makubwa ya ulevi lazima tufanye vizuri zaidi, ulevi huleta mateso makubwa katika familia, vifo vya watoto kabla ya wakati na pia watoto kukua wakiwa wametegwa.”

Vivianne aliongeza kwa kuwaonya watu ambao hawawezi kujizuia kutoka kwa pombe au kuwa na historia ya ulevi kutojiingiza kabisa.

“Kuwa mchekeshaji hakukuniepusha na hilo bali niliacha kucheza nao kwani ni sawa na kucheza na moto utakuchoma tu," alisema.

Akimaliza aliwataka wafuasi wake kushiriki naye jinsi walivyoweza kuacha pombe na kutiana moyo katika  njia za kuishi bila kulewa licha ya msukumo huo.

"Kwa kawaida huanza kama njia ya kujumuika lakini maisha yanapoendelea kuimarika inakuwa rafiki wa wengi wetu.”

“Kupenda pombe ni udanganyifu. Unashtukianga ni miaka 20 na damu imejaa mvinyo Kaeni rada waseee.”