logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Azziad Nasenya:Sipo miongoni mwa wawakilishi watakaozuru michezo ya Olimpiki ,Paris

Azziad pia alidai kuwa ziara yake ya hivi majuzi ya Dubai alijifadhili mwenyewe na wala si kwa usaidizi wa serikali.

image
na Davis Ojiambo

Burudani11 July 2024 - 08:53

Muhtasari


  • •Baadhi ya wakenya walimshtumu waziri Ababu Namwamba kwa kuwajumuisha marafiki zake kwenye orodha hiyo badala ya wanariadha.
  • •Michezo ya Olimpiki kule Paris itaanza Julai 26 na kukamilika Agosti 11,2024

Muunda maudhui ya kidijitali na mtangazaji wa redio Azziad Nasenya amejitokeza wazi kwa madai kuwa yeye ni miongoni mwa  wawakilishi wa Kenya wanaokwenda Paris, Ufaransa kwa michezo ya Olimpiki.

Hii ni baada ya wakenya kumshutumu waziri wa masuala ya vijana, michezo na sanaa Ababu Namwamba kwa kuwajumuisha marafiki zake kwenye orodha hiyo badala ya wanariadha.

Jina la Azziad liliingizwa kwenye mchanganyiko huo, na akatoa maelezo ya kufafanua suala hilo na uhusiano wake na hati hiyo inayoongozwa na Namwamba.

Kupitia ukurasa wake wa X almaarufu Twitter, Azziad alikanusha madai hayo ;

"Mimi si sehemu ya wajumbe wa Kenya kwenye michezo ya Olimpiki ya Paris 2024.Inasikitisha kwamba mtu angeibuka na madai ya uwongo kuhusu suala kama hilo. Kujihusisha kwangu na wizara ya masuala ya vijana, uchumi ubunifu, na michezo kulihusu kamati ya kiufundi ya wabunifu ya baraza la Talanta Hela, inayoongozwa na Daniel Ndambuki, AKA Churchill. Nilichaguliwa na kupewa mamlaka ya kuwakilisha idadi ya vijana katika kamati ya kiufundi ya Ubunifu. Walakini, kamati ilivunjwa mnamo Juni 2023. Sijajihusisha tangu wakati huo," Azziad aliandika.

Kauli ya Azziad inajiri huku kukiwa na shinikizo kutoka kwa baadhi ya wakenya kutaka Waziri Ababu Namwamba aweke hadharani orodha ya watu wasio wanariadha ambao wataandamana na timu ya Olimpiki hadi Paris.

Wakenya watatu wanaitaka wizara hiyo kutoa maelezo kamili ya wanaosafiri, iwapo watatafuta hatua za kisheria. Charleen Njuguna, Jolly Lanji na Baverlyne Kwamboka, kupitia mawakili wao, wameelezea wasiwasi wao kuhusu gharama hiyo kwa walipa ushuru wa Kenya.

Wiki iliyopita, Ababu na Rais William Ruto walipoiaga timu katika Ikulu, alithibitisha kwamba hakutakuwa na nafasi kwa wale watakaoenda tu huko kukaa bila sababu


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved