Trevor asema maoni yake kuwa waunda maudhui hujiuza 'online' hayamlengi 'ex' wake

Trevor aliongeza kwa kusema kuwa mpenzi wake wa zamani Mungai Eve alim'block kila mahali

Muhtasari

•Director Trevor hapo awali aliwashtumu waunda maudhui ya kidijitali hasa wanawake kueka maudhui ya ngono kwenye mitandao ya kijamii ili kupata umaarufu.

•Alijitetea baadaye kwa kusema kuwa maneno hayo hayakuwa yanamlenga ex' wake,Mungai Eve ,hii ni baada ya Eve kutoa kauli yake pia.

Trevor
Trevor
Image: Instagram

Director Trevor ametetea kauli yake aliyotoa kuhusu watayarishaji wa maudhui  ya kidijitali hasa  wa kike wanaounda maudhui ya ngono kwa ajili yakupata umaarufu.

Trevor ameeleza kwamba ujumbe huo haukumhusu mpenzi wake wa zamani,Mungai Eve.Aliongeza kwa kusema kuwa hana nia ya kumzungumzia akidai kuwa mrembo huyo amemzuia kwenye mitandao yake yote ya kijamii na haiwezekani kuona aina ya maudhui anayounda.

"Mungai Eve ni mmoja tu kati ya watayarishaji wengi tulionao Kenya,kwa hivyo siwezi kukaa hivi niseme ana'sexualise' maudhui.Kuna wengi sana.Si vibaya kuunda maudhui ya ngono. Kama yeye ni mmoja wao hata sijui." Trevor alisema.

Hata hivyo aliendelea kwa kusema Mungai Eve amem'block'  kila mahali.

"Siwezi kuona maudhui yake,amenizuia kwa hivyo siwezi kuandika kitu kinachomhusu na huwa sioni  maudhui yake," Trevor alielezea.

Hapo awali,Trevor,Kupitia chapisho kwenye ukurasa wake wa Instagram aliwashtumu waunda maudhui ya kidijitali hasa wanawake ambao wanaunda maudhui ya ngono kwenye mitandao ya kijamii ili kupata umaarufu.

Hata hivyo,mpenzi wa zamani wa Trevor,Mungai Eve hakusita kumjibu Director Trevor.Kupitia mahojiano na wanahabari wa mitandao ya kijamii Eve alisema kuwa kila mtu ana uhuru wa kufanya kile anataka.

"Everybody is entitled to do what makes them happy..life is too short." Mungai Eve alisema. Alipoulizwa ikiwa anam'miss Trevor  alidai kuwa hio ilipitwa na wakati na yeye si mtu wa kurejelea mambo ambayo yalipita.

"Tunaongelea mambo yatakayofanyika baadaye,si mambo yaliyopitwa na wakati.Tulikuwa kwenye mahusiano nzuri wakati ule ,ila kwa sasa kila mtu aendelee na maisha yake." Mungai Eve alisema.