logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Usuli na safari ya msanii Alikiba kimziki

Ali Saleh Kiba almaarufu Alikiba ni msanii wa haiba na wa viwango vikubwa zaidi alizaliwa mnamo Novemba 29,1986 Kigoma Tanzania.

image
na Evans Omoto

Mastaa wako17 February 2025 - 13:34

Muhtasari


  • Katika safari yake ya mziki alikiba ni mwanamziki sifika na kando na kukuwa na uwezo wa kuporomosha magoma mazitomazito Alikiba pia ni mwigizaji,mwelekezaji na mwanasoka Hodari sana.

  Msanii Alikiba

Ali Saleh Kiba almaarufu Alikiba ni msanii wa haiba na wa viwango vikubwa zaidi alizaliwa mnamo Novemba 29,1986 Kigoma Tanzania.

Alikiba pia hujiita jina la msimbo kama King Kiba anamiliki kituo cha King Music na kundi la Crown.Alikiba ni msanii ambaye amesifika sana katika taasinia ya mziki kwa muda  mrefu sana.

Katika safari yake ya mziki Alikiba ni mwanamziki sifika na kando na kukuwa na uwezo wa kuporomosha magoma mazitomazito Alikiba pia ni mwigizaji,mwelekezaji na mwanasoka Hodari sana.

Baadhi ya vibao ambavyo Alikiba amewahi kuvitoa ni kama Mwana,Aje,Chekecha,Nakshi Mrembo,Usiniseme miongoni mwa Vingine vingi.Alikiba ni msaani ambaye amevuma sana kimziki na kutwaa zawadi na tuzo kochokocho ndani na nje ya Tanzania.

Ulipofika mwaka wa 2011 Alikiba alijipa mapumziko mafupi kisha akarudi 2014 na kibao Mwana, kibao ambacho kilivuma na kupokelewa vyema na mashabiki waliopendezwa na mahadhi yake kisauti na ujumbe mzito uliokuwa humo ndani.

Jambo ambalo lilisababisha kutuzwa na kupokea zawadi kochokocho zaidi ya tuzo 5.

Katika orodha hiyo kibao chake cha AJE kilirodheshwa nambari 3 katika nyimbo mia moja za Tanzania 2012-2022.

Alikiba alishirikiana na wasanii mbalimbali kuhakikisha kuwa anaimarisha kipaji chake vyema na kuhakikisha kuwa kila kitu kinamuendea shwari baadhi ya wasanii ambao aliwahi kushirikiana nao ni kama Partoranking,Sauti Soul, Mario na Nyashisiki.

Alikiba kwa maisha yake kimziki amekuwa akipiga hatua ya ufanisi muda baada ya muda, mnamo mwaka wa 2021 Kiba alizindua studio mpya na kuwa na albamu ambayo aliita Mfalme mmoja ambayo ilikuwa imebeba nyimbo 16.

Mnamo mwaka wa 2022, Alikiba alishinda tuzo kadhaa tuzo ikiwemo ya msanii bora, tuzo ya mwanavideo na mwanamziki bora nchini ni baadhi ya tuzo ambazo nguli huyu kimziki amezitwaa na kuwa mfalme wa sanaa hii murwa.

Oktoba 3, 2024  Alikiba alizindua steshini yake mpya ya redio  kwa jina  Crown fm 92.1 , Kituo ambacho mawimbi yake yanashika Tanga, Pwani, Zanzibar, Dar es Salaam na Tanga.

Kwa hivyo bila shaka msanii Alikiba amekuwa kielelezo chema na mfano bora na hai wa kuigwa.

Kwa miezi ambayo imepita Alikiba amekuwa akishirikiana  na msaani Darassa katika kolabo ya kucharaza vibao motomoto.

Alikiba anasalia kuwa miongoni mwa wasanii ambao malengo yao yako juu na wanatumia mziki jinsi inavyostahili ili kuwalea wasanii chipukizi.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved