logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Safari ya msanii Masauti kimziki

Mohammed Ali Said alimaarufu Masauti ni msanii wa Kenya aliyezaliwa Mombasa Kenya.

image
na Evans Omoto

Mastaa wako20 February 2025 - 15:30

Muhtasari


  • Masauti ni msanii wa haiba ambaye anawakilisha kizazi cha leo Katika mziki wa bongo.
  • Katika umri wake akiwa mdogo Masauti alipenda sana kuwasikiliza wasanii mbalimbali Pamoja na kujitungia nyimbo za kuimba. 

Safari  ya msanii Masauti

Mohammed   Ali  Said almaarufu Masauti ni msanii wa Kenya aliyezaliwa Mombasa Kenya.

Masauti ni msanii wa haiba ambaye anawakilisha kizazi cha leo Katika mziki wa bongo. Msanii Masauti safari yake ya masomo ilikatizwa kutokana na ukosefu wa karo kumwezesha kuendeleza  masomo yako.

Katika umri wake akiwa mdogo Masauti alipenda sana kuwasikiliza wasanii mbalimbali Pamoja na kujitungia nyimbo za kuimba. Mara si mara alikuwa akizuru studio mbalimbali akiandamana na wasanii wenzake ili kuvinjari mazingira ya studio.

Hapo ndipo Masauti alishikwa na uchu na ari ya kuanza kuimba akawa akiijiita mswazi Masauti kijana mwenye kipaji cheupe tena mwenye ubunifu mkubwa.

Itakumbukwa wazi kuwa masauti alianza kuimba akiwa na umri wa miaka kumi na mitatu katika umri wake huo alikuwa kijana machachari  tena mpwamu na mneni sana mbele ya halaiki.

Hatimaye Masauti aliweza kugura kutoka Mombasa kisha akaenda Nairobi akiwa Nairobi aliendeleza injili ya usanii na kutambulika sana na watu mbalimbali kisha akajisajili na msanii Teddy Josiah ambapo alikuja akatambuliwa na Jalango mwaka wa 2019.

Jalango alimpokea masauti na kumpa nafasi siku moja katika Redio huku akishirikiana na wasanii kama Khaligraph Jones wasanii waliomuandalia mkeka wa makuzi na kumpa malezi bora kama msanii chipukukizi.

Masauti baada ya kuvalia magwanda rasmi ya  mziki na kuwa msanii mwewnye malengo mapana baada ya kuporomosha ngoma kali  na kujiweka katika viwango vikubwa  alianza kuwa kipenzi cha wengi wakiwemo pia mabinti waliommezea mate msanii Masauti.

Kuna  siku tetesi zilisema kuwa  alikuwa kipenzi  cha  msanii Nadia Mukami kutokana na ujio mpwa tena wenye nguzu aliokuwa nao akachukua mtindo wake kisanaa na kujitambua sana.

Baadhi ya vibao ambavyo msanii masauti amevicharaza ni  Ipepete,Sokote,Dondosha,liar,Inauma,Pepo na Sare na kuonekana kidedeakatika taasinia hiyo ya mziki.

Msanii Masauti ni msanii mmojawapo  ambaye anaiweka safu ya wasanii bora nchini kwa kuimba na kupanua mawanda ya mziki hadi ukanda wa afrika mashariki kwenye mitandao ya kijamii hasa ule wa instagram ana mashabiki elifu mia tatu tisini na wa tatu 393,000.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved