logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Usuli na Safari ya Msanii Madini Classic

John Philip Ouma alimaarufu msanii Madini Classic ni msanii wa Bongo Mkenya mzaliwa wa Kisumu.

image
na Evans Omoto

Mastaa wako28 February 2025 - 15:09

Muhtasari


  • Alizaliwa mnamo Desemba 2,1994 katika gatuzi la Kisumu mkoa wa Nyanza Japo aligura na Kwenda nchi ya Tanzania wakati ambapo kipaji chake cha usanii kilichipuka.
  • Katika hali yake ya Udogo na ujana Madini alikuwa akiimba na kurekodi nyimbo kadhaa ila alikosa mtaji wa kurekodi video akawa ametulia chini ya zulia.

John Philip Ouma alimaarufu msanii Madini Classic ni msanii wa Bongo Mkenya mzaliwa wa Kisumu.

Alizaliwa mnamo Desemba 2,1994 katika gatuzi la Kisumu mkoa wa Nyanza Japo aligura na Kwenda nchi ya Tanzania wakati ambapo kipaji chake cha usanii kilichipuka.

Baada ya muda Madini alirudi nchini Kenya na kuka upande wa Pwani,alianza safari yake ya usanii akiwa mdogo alipokuwa akijifunza kuimba miziki aina ya bongo.

Katika hali yake ya udogo na ujana Madini alikuwa akiimba na kurekodi nyimbo kadhaa ila alikosa mtaji wa kurekodi video akawa ametulia chini ya zulia akisubiri hali imwendee nyema kihela.

Madini classic alipagazwa jina MADINI kutoka kwa babu yake  aliyekuwa anafanya kazi nchii ya Tanzania ambaye alikuwa mchimba migodi mahiri na madini kule Taifa la Tanzania.

Katika safari yake ya muziki madini classic alivicharaza vibao kadha ambavyo vilimkweza na kumuweka katika safu ya wasanii bora ukanda wa Afrika Mashariki na Kati hadi upande wa janga la Sahara na baadhi ya sehemu za Mto Limpopo.

Baadhi ya Vibao ambavyo Madini ameviachilia ni Nitalewa,Taratibu,Goma,Toto la Kanairo,Bingo Bango,Tawire miongoni mwa vibao mbalimbali ambavyo vilihanikiza na kuteka anga kwa mirindimo ya kipekee.

Katika mahojiano na kituo cha Habari cha Mpasho Madini aliwahi sema  na kusadiki kuwa mara nyingi yeye huwa hapendi kuishi maisha ya bandia ili ifahamike na watu kuwa hali yake ya Maisha i sawa kumbe la.

Madini alielelezea kuwa katika safari yake ya muziki na maisha yake kwa jumla hajawahi kuazia kujihusisha na maisha ya kughushi katika hali  halisi ya hapa duniani yeye hukiri na kususia lile  ambalo anahisi haliko sawa ila si kufurahisha umma  jinsi wasani wengi kwa asilimia kubwa  wanavyofanya.

Madini kutokana na mujibu wa maelezo yake alisema kuwa mara nyingi wasanii wengi huwa na hulka ya  kutaka sifa na majitapo na kutaka kujulikanaa hivyo kuishia kufanya  vitu ambavyo ni kinaya cha kuogofya na uhalisia wa maisha yao.

Kulingana na kujitambua huko  kwa Madini ndiko kumempa jina kubwa  jina ambalo limejulikana na kupata umaarufu wa hali ya juu sana.

 Msanii Madini Classic unaposikiliza vibao vyake utagundua kuwa ni msanii ambaye amezamia kwa lugha ya Kiswahili sanifu yeye ni msanii ambaye ni mtunzi mzuri wa Mashairi ambayo huwa na ujumbe kwa jamii katika viwango vyote  si elimu, kilimo ,biashara,siasa na mapenzi  ujumbe huwa  huwa umekolea sana.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved