Msanii Melody aliandika kwenye ukurasa wake wa Instagram akiwaonea huruma wazazi wanaowatenga wanao hasa uja uzito unapotokea bila kupangwa.
Amesisitiza kwamba ni vyema kuonesha upendo kwa mwanao na akifanikiwa kwa siku za baadaye huenda akarejesha mkono tofauti kabisa na iwapo wataweatengwa wanao.
"Kama umepata mtoto, iwe hukupenga au vyovyote vile, usifanye kosa la kutokumulea huyo mtoto. Baadae mtoto akiwa na maisha yake utaleta lawama na yeye hatokujali kama ulivyofanya. wazee tulee watoto wetu. watoto ni baraka," alindika mwanamziki Melody.
Jay Melody ambaye kwa sasa Machi 2025 ana umri wa miaka 28, kando na kuwa mwimbaji ni mwandishi wa nyimbo. Ameimbaa vibao kadhaa vikiwemo, Nakupenda, Sawa, Wa pekee yangu, Nitasema, miongoni mwa vibao vingine.
Mwaka 2016 ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Jay Melody kuingia katika tasnia ya muziki alipojiunga na chuo kikuu cha Tanzania House of Talent (THT).
Baada ya mwaka mmoja wa kujifunza muziki Jay Melody hatimaye alisainiwa na Epic Records Tanzania moja ya lebo kubwa za rekodi nchini zinazomilikiwa na Genius Ruge Mutahaba na kuwaachiwa wimbo wake wa kwanza unaokwenda kwa jina 'Goroka'
Mwanamziki huyo wa bongo pia amefanya kolabo kadhaa na wasanii wakubwa nchini Tanzania akiwemo kiongozi wa Wasafi Diamond Platinumz.