logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Rayvanny anataja umri mdogo wa Fahymah kama chanzo cha kuchelewesha ndoa yao

Fahymah na Rayvanny hawajawahi kuachana rasmi tangu kuanza mahusiano yao.

image
na Japheth Nyongesa

Mastaa wako20 March 2025 - 09:36

Muhtasari


  • Rayvanny alitaka kumuoa mwanadada wake Fahymah zamani ila umri wake mdogo ulichangia pakubwa ndoa hiyo kuchelewa.
  • Mwanamuziki huyo aliweka wazi kwamba hayuko tayari kumpoteza Fahymah.

Rayvanny and his lover Fahymah
Mwanamuziki wa bongo Rayvanny tokea nchini Tanzania sasa amefunguka kwamba alitaka kumuoa mwanadada wake Fahymah zamani ila umri wake mdogo ulichangia pakubwa ndoa hiyo kuchelewa.

Kwenye mazungumzo na wanahabari amekiri kwamba yeye alianza mipango ya kufunga ndoa na mrembo huyo pindi tu baada ya kukutana ila Fahymah hakuwa tayari kwani alihofia kwamba angali mdogo kiumri.

"Mwaka wa kwanza nimeanza naye, nilikuwa na moto sana. Ata sijatoka, kwetu wajatoka ivo, nishaanza kupanga mipango. Ila nakwambia akakataa akisema mimi bado mdogo. Nikamwambia vipi bwana nioe akasema apana mimi bado mdogo, ngoja kwanza subiri nikamwambia sawa," alifichua Rayvanny.

"Nikamwambia sawa, vitu vitakuwa vizuri acha tungoje muda. Nafikiria kwa sasa hivi niko tayari na mwenyewe pia amefurahi kwa hili. Mwanamke kuolewa ni furaha. Alafu pia marafiki, unapoona watu wake wengi wa pembeni, marafiki wake wengi unajua.. bwana akuoe. Ila mimi siowi kwamba nalazimishwa. Naoa kwa sababu mimi nataka," aliweka wazi.

Msanii Rayvanny amemsifia mrembo wake Fahymah huku akimtaja kama mwanamke wa kipekee na tabia za kupendeza mwenye akili ya kutatua mambo kwa njia nzuri. Ameeleza kwamba ni mwanadada ambaye hana hasira na anajua kutatua mambo.

"Fahymah ni mwanamke ambaye ni mvumilivu, ni mwanamke ambaye anaweza kukuletea heshima. Akiwa na asira siyo mwanamke ambaye anaweza tenda matukio ya kukuudhi. Kwa hivyo ukimpoteza mtu wa namna hiyo... Unajua unapomfanyia mwanamke vitimbwi, anapata mshauri na anakutana na vishawishi vingi," alieleza Rayvanny.

Mwanamuziki huyo aliweka wazi kwamba hayuko tayari kumpoteza Fahymah kwani ni chaguo lake na yuko na kila sababu za kumheshimu.

'Mtu ambaye anaweza akawa upande wako akakuletea heshima. anahakikisha hauchafuki kwenye umati mheshimu. Sio watu wote wanaweza hilo," alisema mwanamuziki huyo wa lebo ya Next Leval Music.

Fahyvanny ambaye ni mpenzi wa mwimbaji  huyo maarufu wa Tanzania ni mzaliwa wa nchi hiyo ya Tanzania. Yeye na Rayvanny hawajawahi kuachana rasmi tangu kuanza mahusiano yao.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved