logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Zuchu aahindi kumng'ang'ania Diamond mpaka dakika ya mwisho

Wakati huo pia ameeleza kwamba ana imani kwamba Diamond anampenda na pia anamung'ang'ania.

image
na Japheth Nyongesa

Mastaa wako28 March 2025 - 10:47

Muhtasari


  • Ameweka wazi kwamba anampenda Diamond na hayuko tarari kumpoteza akiahidi kumung'ang'ania mpaka mwisho.
  • "Kama wewe ni mwanamke unajiamini kwamba Diamond ni mwanaume wako jitokeze tuone," aliweka wazi mwanamuziki huyo.
Diamond Platinumz and Zuchu
Mwanamuziki wa bongo Tanzania Zuhura Othman maarufu Zuchu sasa anasema kwamba yupo tayari kupigana vita visivyokamilika ili kutwaa moyo wa mwanamziki Diamond platinumz.

Zuchu kwenye mahojiano na mwanahabari ameweka wazi kwamba anampenda Diamond na hayuko tarari kumpoteza akiahidi kumung'ang'ania mpaka mwisho.

Wakati huo pia ameeleza kwamba ana imani kwamba Diamond anampenda na pia anamung'ang'ania.

Nasikia raha kushinda nikimng'ang'ania mpenzi wangu. Sidhani kama kuna mwanamke anaeza hilo, kama yuko sidhani. Nasikia raha sana kumng'ang'ania. Mimi ni king'ang'anizi na nitamung'ang'ania mpaka mwisho. Raha ya Kung'ang'ania siku zote nasema ni wewe pia ung'ang'aniwe. Sio kung'ania usipong'ang'aniwa. Mimi na Diamond tunang'ang'aniana, " alieleza

Mwanadada huyo pia anamtaka mrembo yeyote anayejiamini kwamba Diamond ni mpenzi wake ajitokeze hadharani wakutane.

"Kama wewe ni mwanamke unajiamini kwamba Diamond ni mwanaume wako jitokeze tuone," aliweka wazi mwanamuziki huyo wa kibao cha Napambana.

Zuchu ambaye amekuwa mpenzi wa mwanamuzuiki Diamond kwa muda sasa ni mwanamuziki wa lebo ya Wasafi ambayo inamilikiwa na huyo mpenzi wake.

Wanamuziki hao wawili waliweka wazi mahusiano yao ya kimapenzi mwezi novemba 2022 baada ya uvumi huo kuwepo kwa muda mrefu kabla ya hapo.

Mwanamuziki Zuchu alianza kuvuma na kuteka anga za utumbuizaji baada ya kujiunga na wasafi, jambo ambalo linatajwa kwamba zilikuwa juhudi za mama yake mzazi kuwaunganisha na Diamond ili amshike mkono.

Licha ya kwamba Zuchu ana mapenzi ya dhati mwa rais huyo wa Wasafi, wafwasi wao wanabaki na maswali chungu nzima iwapo atafaulu kumutuliza Diamond kwani ni mmoja kati ya wanamuziki ambao wamefaulu kupenndwa na wanawake wengi.

Baadhi ya wanawake warembo na maarufua ambao walijaribu kumkaba Diamond ila hawakufaulu ni pamoja na Hamisa Mobeto, Wema Sepetu, Zari Hassan na Tanasha Donna.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved