logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Leo ama Kesho nitakufa ila matendo yangu yataongea - Diamond Platinumz

Diamond Platinumz sasa anaeleza kwamba yuko kipaumbele kutenda mema.

image
na Japheth Nyongesa

Mastaa wako01 April 2025 - 09:20

Muhtasari


  • Kiongozi huyo wa lebo ya Wasafi pia aliweka wazi kwamba kama wanadamu wanafaa kusaidiana.
  • Eid ul Fitr ni sikukuu ya kidini kwa Waislamu wote duniani kote.
Diamond Platinu8mz Sharing gifts during Eid Ul Fitr
Mwanamuziki tajika wa bongo nchini Tanzania Diamond Platinumz sasa anaeleza kwamba yuko kipaumbele kutenda mema kwa wanadamu huku akiamini kwamba ipo siku mema yatanena.

Diamond alikuwa anazungumza haya kwenye mahojiano na mwanahabari baada ya kuanzisha shughuli za ugavi wa misaada kwa baadhi ya wananchi wa Tanzania wakati wa maadhimisho ya  Eid ul Fitr 2025.

"Niko na shughuli kule, viongozi tunagawa misaada, mimi nimemaliza nimeachia vijana waendelee na hiyo shughuli sasa," alisema Diamond.

Kiongozi huyo wa lebo ya Wasafi pia aliweka wazi kwamba kama wanadamu wanafaa kusaidiana bila ubaguzi maana kila wakati kila mmoja anamhitaji mwenzake.

"Nimefika hapa kwa sababu ya undugu, unajua lazima uishi na watu vizuri. Hii dunia tunapita. Kuna siku sitakuwepo mambo yangu ndo yatazungumza. Kuna siku nitakuwa na shinda na nitawahitaji kwa hivyo lazima tuishi pamoja kusaidiana na kutegemeana bila kumdharau mtu,"  Alieleza zaidi.

Mwanamziki huyo maarufu Tanzania na Afrika mashariki ni miongoni mwa wanamziki ambao walijitokeza kusherehekea pamoja na ndugu waisilamu katika maadhimisho ya Eid ul Fitr.

Eid ul Fitr ni sikukuu ya kidini kwa Waislamu wote duniani kote. Eid al-Fitr inaashiria mwisho wa mwezi mtukufu wa Ramadhani. Eid al Fitr ni thawabu ya Mwenyezi Mungu kwa waumini waliofunga wakati wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Hawa pia ni waumini wanaomshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuwapa nafasi na nguvu za kutekeleza amri zake wakati wa mwezi uliobarikiwa wa Ramadhani. Kijadi, Eid al Fitr huadhimishwa kwa siku tatu katika karibu nchi zote za Kiislamu.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved