logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Gidi aahidi kusaidia kuboresha alikokuwa akiishi Dandora baada ya kufanya ziara (+picha)

Wakazi wa Dandora walimueleza  Gidi matatizo yanayowakumba na akahidi kufuatilia.

image
na Radio Jambo

Habari26 September 2022 - 08:02

Muhtasari


•Gidi alitumia ziara yake kutembelea shule ya msingi aliyosomea, nyumba yake ya zamani ya kukodisha na pia kutangamana na baadhi ya marafiki wake wa zamani.

•Baadhi ya mashabiki ambao alitangamana nao walisikika wakiuliza alikomwacha mtangazaji mwenzake Ghost Mulee.

Siku ya Jumapili mtangazaji wa kipindi cha Gidi na Ghost Asubuhi kwenye Radio Jambo Joseph Ogidi almaarufu Gidi alizuru mtaa wake wa kuzaliwa wa Dandora, jijini Nairobi.

Gidi alitumia ziara yake kutembelea shule ya msingi aliyosomea, nyumba yake ya zamani ya kukodisha na pia kutangamana na baadhi ya marafiki wake wa zamani.

Wakazi wa Dandora walitumia fursa hiyo kueleza baadhi ya matatizo yanayokumba eneo hilo na baada ya kuwasikiliza mtangazaji huyo mahiri akahidi kufuatilia.

"Ilikuwa ni nyakati za kihisia kutembelea mtaa nilikozaliwa na kukulia DANDORA PHASE 4. Ahsante sana watu wa D kwa makaribisho. Kwa vijana, nimesikia kero zenu nitatumia ushawishi wangu kuboresha mtaa wetu," Gidi alisema kupitia ukurasa wake wa Instagram.

Aliahidi kuanza kwa kuzungumza na gavana wa Nairobi Johnson Sakaja ili kufungua uwanja wa Dandora hivi karibuni ili vijana wa eneo hilo wapate mahali pazuri pa kufanyia mazoezi na kushiriki michezo mbalimbali.

Mtangazaji wa kipindi cha asubuhi alifurahi kutembelea iliyokuwa shule yake ya msingi na kuyaona baadhi ya madarasa ambayo alisomea. Pia alipata fursa ya kukutana na mwalimu mkuu wa sasa wa shule hiyo.

Katika moja ya video alizochapisha, Gidi alionekana akionyeshana nyumba ambayo alikuwa akiishi zamani katika mtaa huo.

"Hii ndiyo nyumba ya kwanza niliyoishi nilipokuja Nairobi. Hapa ndipo nilipoishi, ni nyumba ya vyumba viwili," alisema. 

Pia alionyesha eneo la burudani alilopenda kutembelea wakati alipokuwa akiishi pale.

Tazama picha za Gidi akitangamana na mashabiki wake mtaani Dandora Phase IV  chini hapa:-

Baadhi ya mashabiki ambao alitangamana nao walisikika wakiuliza alikomwacha mtangazaji mwenzake Ghost Mulee.

"Ghost yuko.. nashukuru" alimjibu shabiki mmoja aliyeeleza upendo wake kwa kipindi cha Gidi na Ghost asubuhi.

Gidi alizaliwa na kukulia katika mtaa wa Dandora kabla ya kujiunga na shule ya upili ya Aquinas kisha kuendeleza masomo yake katika vyuo kikuu cha JKUAT na KCA.

Kabla ya kujiunga na Radio, Gidi alifanya kazi katika Umoja wa Mataifa na pia alikuwa mwanamuziki. Alikuwa kwenye kundi la Gidi Gidi Maji Maji.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved