logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Ogopa wanawake,'Crazy Kennar asema katika ujumbe wa kimafumbo

Crazy Kennar siku zote amekuwa moja kwa moja katika kueleza hisia zake

image
na Radio Jambo

Burudani09 January 2023 - 09:13

Muhtasari


  • Wakenya wameibua wasiwasi kuhusu kile kinachoweza kuwa kinaendelea kwa Crazy Kennar kufuatia ujumbe wake wa kimafumbo ambao umeenea mitandaoni

Crazy Kennar ni mtayarishaji maudhui maarufu nchini Kenya. Amekuwa akitumia mtandao kuonyesha mbwembwe na maudhui yake ya kibunifu ambayo yamekuwa yakivuma kila mara na kuzua kicheko miongoni mwa Wakenya na hivyo kuondoa huzuni.

Crazy Kennar siku zote amekuwa moja kwa moja katika kueleza hisia zake na heka heka zake akiwa katika tasnia ya burudani.

Katika tukio la hivi punde, Wakenya wameibua wasiwasi kuhusu kile kinachoweza kuwa kinaendelea katika maisha ya Crazy Kennar kufuatia ujumbe wake wa kimafumbo ambao alichapisha mitandaoni.

Katika chapisho la hivi punde zaidi, Crazy Kennar amewaacha mashabiki wake katika hali ya kuchanganyikiwa huku wakishindwa kile ambacho wanawake wamemfanyia kufuatia chapisho lake akitahadharisha watu kuhusu wanawake.

Kupitia kwenye ukurasa wake rasmi wa Instagram aliandika;

"Ogopa wanawake Wooiii hata hangengoja january ifike tarehe 15 πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚,"Kennar Aliandika.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logoΒ© Radio Jambo 2024. All rights reserved