logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mtangazaji Catherine Kasavuli avunja kimya baada ya kulazwa kutokana na saratani

Pia kwenye ujumbe wake wamesema kuwa anamatumaini haya yote atapambana nayo.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri07 November 2022 - 09:04

Muhtasari


  • Gwiji huyo wa utangazaji wa habari amelazwa katika hospitali ya Kenyatta baada ya kugundulika kuwa na saratani ya shingo ya kizazi (Cervical Cancer)

Mtangazaji Catherine Kasavuli amezungumza baada ya ombi la damu kutolewa ili kurejesha afya yake.

Kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram mtangazaji huyo wa kituo cha KBC, amewashukuru mashabiki kwa maombi yao na jumbe zao za kumtia moyo.

Pia kwenye ujumbe wake amesema kuwa anmatumaini ataweza kupambana na yote yanayomkabili. 

"Asanteni kwa maombi yenu na jumbe zenu za kutia moyo, tutapambana na hili," aliandika Kasavuli.

Kituo cha Runinga cha Kitaifa cha KBC Channel 1 pia kimefanya ombi la msaada wa damu kwa ajili kwa mfanyakazi huyo wake kupitia kurasa rasmi za mitandao ya kijamii.

"Mtangazaji mkongwe Catherine Kasavuli amelazwa katika Hospitali ya KNH, Mrengo wa Kibinafsi baada ya kugundulika kuwa na saratani ya shingo ya kizazi. Kundi lolote la damu litafanya," taarifa ya KBC ilisoma.

Gwiji huyo wa utangazaji wa habari amelazwa katika hospitali ya Kenyatta baada ya kugundulika kuwa na saratani ya shingo ya kizazi (Cervical Cancer).

Wanamitandao na mashabiki walitaia afueni ya haraka na hizi hapa baadhi ya jumbe zao;

jahmbykoikai: Wishing you a quick recovery and total healing in Jesus name ma'am❤️. We shall fight this and you will overcome. I love you mama❤️

djshiti_comedian: Wishing You Quick revovery ... You are a true worrior Madam Cate... Natabiri Uponyaji juu ya Maisha Yako Katika Jina La YESU.🔥🔥🔥🙌🙌🙌

_june.c_: Quick recovery Mama,stay strong❤️ so much love

paulinevulimu: Praying for you mama...much love and hugs for you❤️❤️


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved