logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Stevo, mkewe wajawa bashasha baada ya mbunge Salasya kuwapa makazi ya heshima

Peter Salasya mnamo Jumanne alitimiza ahadi yake kwa mwimbaji Stivo Simple Boy ya kumpatia makazi ya heshima.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri05 July 2023 - 08:02

Muhtasari


•Peter Salasya mnamo Jumanne alitimiza ahadi yake kwa mwimbaji Stivo Simple Boy ya kumpatia makazi ya heshima.

•Salasya alisema kuwa yuko tayari kumsaidia Stivo Simple Boy iwapo atafikiria kujitosa katika kazi zingine za kutengeneza pesa mbali na muziki.

Mbunge wa eneo la Mumia East, Peter Salasya mnamo Jumanne alitimiza ahadi yake kwa mwimbaji Stevo Simple Boy ya kumpatia makazi ya heshima.

Mwanasiasa huyo kijana aliwapeleka Stevo na mke wake Grace Atieno hadi kwenye nyumba aliyowatafutia jijini Nairobi na kuthibitisha kwamba tayari alikuwa amemaliza kuilipia kodi.

Akizungumza na mwanahabari Presenter Ali ambaye alikuwa ameandamana na watatu hao kwenye ziara ya nyumba hiyo, Salasya alisema kuwa mke wa mwimbaji huyo kutoka Kibra alimthibitishia kuwa nyumba hiyo ni sawa kwao.

“Nilimuuliza mke wake ‘umependa hiyo place?’.. Bibi ndiye huwa anaamua. Alisema iko juu. Nikasema kama ashasema iko juu, iko sawa nikalipa. Kila kitu kiko sawa,” Salasya alisema.

Mbunge huyo wa muhula wa kwanza alithibitisha kuwa atamrudisha Bi Atieno shuleni kwa kozi fupi ya masuala ya urembo ili awe na ujuzi utakaomsaidia kukidhi mahitaji yake na kusaidia familia yao ndogo.

“Nitamlipia shule ili aweze kujikimu. Pia nitamfungulia duka la nguo ili aweze kujisimamia ili bwana akienda shoo akipata ama asipopata kwa nyumba bibi atakuwa sawa. Wawe wanasaidiana,” Salasya alisema.

Aidha, Salasya alisema kuwa yuko tayari kumsaidia Stivo Simple Boy iwapo atafikiria kujitosa katika kazi zingine za kutengeneza pesa mbali na muziki.

"Pia nilisema wale ambao waliahidi kumjengea kama hawatafanya hivyo ndani ya siku 15 zijazo nitaenda Oyugis nimtengezee nyumba huko alafu aanze hapo," alisema mbunge huyo.

Mkewe Stevo, Bi Atieno alimshukuru mwanasiasa huyo kijana ambaye pia aliahidi kuwapa shilingi elfu 30 ili kununua baadhi ya vitu vya nyumbani.

Rapa Stivo pia alimshukuru mbunge huyo na kuahidi kufanya kazi pamoja naye.

Mbunge Salasya alisema kuwa kesi ya Stevo Simple Boy ilimgusa kwani aliiona ni ya kweli na ilimkumbusha nafasi aliyokuwa nayo kabla ya kuwa mbunge mwaka jana.

Salasya alikutana na msanii huyo aliyekabiliwa na misukosuko mingi kwenye safari yake ya muziki siku chache zilizopita amba aliahidi kumhamisha.

Alikuwa ameomba kukutanishwa na msanii huyo kutoka Kibera baada ya hadithi yake kuenezwa kuanzia wiki jana jinsi amekuwa akipitia maisha magumu hadi kulala njaa licha ya kuwa na jina kubwa kwenye Sanaa.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved