logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Zuchu alazimika kusitisha shoo baada ya kurushiwa jiwe usoni akiwa kwenye steji

Zuchu had just greeted the fans and was preparing to perform when a stone landed on his face.

image
na Radio Jambo

Habari30 September 2023 - 13:25

Muhtasari


•Zuchu mnamo siku ya  Ijumaa jioni alilazimika kusitisha shoo yake kwa muda baada ya kupigwa na jiwe usoni.

•Walinzi waliokuwa wamesimama karibu walionekana wakimuelekeza kutoka jukwaani hadi mahali pa usalama huku kelele zikiongezeka kutoka kwa umati.

Malkia wa Bongo Zuhura Othman almaarufu Zuchu mnamo siku ya  Ijumaa jioni alilazimika kusitisha shoo yake kwa muda baada ya kupigwa na jiwe usoni.

Msanii huyo wa WCB alipanda jukwaani kutumbuiza na alipokuwa akiwasalimia mashabiki waliojitokeza kwenye tamasha la VIP-Pre-Party lililofanyika mjini Mbeya, Tanzania, jiwe lililorushwa kutoka kwenye umati  lilitua usoni mwake

“Mbeya mambo..” Zuchu alisikika akiwaambia mashabiki kabla ya kusimama mara moja na kuinamisha uso wake chini baada ya kugongwa.

Walinzi waliokuwa wamesimama karibu walionekana wakimuelekeza kutoka jukwaani hadi mahali pa usalama huku kelele zikiongezeka kutoka kwa umati.

Baada ya kufanyiwa tathmini na kuthibitishwa kuwa hakujeruhiwa vibaya na jiwe hilo, mwimbaji huyo mzaliwa wa Zanzibar alirejea jukwaani na kuendelea kuwapa raha mashabiki wake kwa vionjo vya nyimbo zake nzuri ukiwemo wa hivi majuzi wa ‘Honey.

WCB walikuwa wameandaa shoo iliyopewa jina la ‘’V.I.P PRE-PARTY'  katika City Pub Mbeya kabla ya tamasha la Wasafi Festival lililopangwa kufanyika siku ya Jumamosi jioni. Karamu hiyo ilipambwa na wasanii waliopangwa kutumbuiza kwenye tamasha la Wasafi Festival, toleo la Mbeya .

Wasanii wengine waliotumbuiza kwenye pre-party hiyo ya Ijumaa jioni ni pamoja na bosi wa WCB, Diamond Platnumz, Lavalava na Mbosso ambao wote wapo chini ya Wasafi Records. Wanne hao walipiga shoo la kusisimua na mashabiki walisikika wakiwashangilia walipokuwa wakipanda jukwaani mmoja baada ya mwingine.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved