Itumbi amekuwa akihudhuria vikao vya kesi ya mauaji inayomkumba Maribe na mpenziwe wake wa zamani Joseph Irungu ,na masaibu yaliomfika ,jumatano yalitoa fursa kwa mwanahabari huyo kwenda kumwona .
Maribe na Jowie wanakabiliwa na kesi ya mauaji ya mfanyibiashara Monica Kimani katika nyumba za Lamuria Gardens mwaka wa 2018 . Maribe na Itumbi wana historia ndefu lakini iliyoghubika usiri kuhusu hali ya uhusiano wao sasa kwani kwa wakati mmoja walidaiwa kuwa wapenzi .