logo

NOW ON AIR

Listen in Live

4 waangamia katika ajali ya barabarani

4 waangamia katika ajali ya barabarani

image
na

Habari02 October 2020 - 02:40
Wafanyibiashara wanne waliuawa siku ya Jumatano baada ya lori lililokuwa likiendeshwa kwa kasi kuwakanyaga katika barabara kuu ya Nairobi – Nakuru karibu na eneo Soko Mjinga.

Watu wengine 10 walijeruhiwa, watano kati yao malipata majeraha mabaya na kupelekwa katika hospitali ya Kaunti ndogo ya Naivasha.  Shughuli za kawaida katika soko hilo zililemazwa huku polisi wakifika kuchukua miili ya walioaga na kuvuta mabaki ya magari yaliohusika katika ajali hiyo.

Kulingana na mfanyibiashara katika soko hilo, Jackson Mwangi, kwanza lori hilo liligonga matatu iliokuwa ikibeba abiria na gari lingine dogo.

“Tukio lilifanyika haraka sana,” alisema

OCPD wa Njabini Charls Rotich alisema kwamba dereva wa lori hilo alitoweka na polisi wameanzisha msako kumtafuta.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved