logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Patanisho: Alitoka nyumbani bila sababu mwaka 2017

Patanisho: Alitoka nyumbani bila sababu mwaka 2017

image
na

Habari02 October 2020 - 02:59

Bi. Emily alipiga simu akitaka kupatanishwa na mumewe,Fredrick aliyemwacha mwaka wa 2017. Wawili hawa wana mtoto mmoja mwenye umri wa miaka mitatu na nusu.

 "Tulikuwa tumeishi vizuri na mume wangu lakini mwaka wa 2017 nilianza kuona tabia za kiajabu kutoka kwakee. Alianza kuja nyumbani kama amechelewa sana kitu saa nane usiku na akifika anasema ameshiba. Siku moja nilimwambia  kimchezo kama amechoka na mimi achukue virago vyake na aende zake. La kustaajabisha alichukua vitu na akaenda na hadi wa leo hajawahi kurudi."

Emily amekua akizungumza na mumewe hata ikafikia kuwa mumewe anamtumia pesa kila wakati akimwitisha licha ya kwamba mumewe huyo amekataa kurudi nyumbani.

Tulipompigia bwana Fredrick simu alikataa kuzungumza nasi kwani alisema kuwa atampigia mkewe simu baadaye.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved