Bi. Emily alipiga simu akitaka kupatanishwa na mumewe,Fredrick aliyemwacha mwaka wa 2017. Wawili hawa wana mtoto mmoja mwenye umri wa miaka mitatu na nusu.
Emily amekua akizungumza na mumewe hata ikafikia kuwa mumewe anamtumia pesa kila wakati akimwitisha licha ya kwamba mumewe huyo amekataa kurudi nyumbani.
Tulipompigia bwana Fredrick simu alikataa kuzungumza nasi kwani alisema kuwa atampigia mkewe simu baadaye.