logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Machifu wakamatwa Wajir wakiongeza idadi ya watu katika Sensa

Machifu wakamatwa Wajir wakiongeza idadi ya watu katika Sensa

image
na

Habari02 October 2020 - 03:02
CENSUS
#WajirCensusFraud ilitamba kwenye twitter siku ya Jumanne baada ya wakenya kulalamikia kuhusu uhalali wa zoezi linaloendelea la kuhesabu watu.

Wakenya katika twitter walitilia shaka zoezi zima la kuhesabu watu baada ya afisa mmoja wa kuhesabu watu kupatikana amesajili watu 600 badala ya idadi iliolengwa ya watu 100. Hii wanaamini ni njama ya wanasiasa kuongeza idadi ya watu katika maeneo wanamotoka kwa manufaa ya kisiasa, hasa katika maeneo yenye watu wachache na wanao kaa mbali mbali.

Hii inajiri siku moja baada ya machifu wawili na naibu wa chifu katika eneo la Wajir kutiwa mbaroni kuhusiana na ulaghai katika zoezi la kuhesabu watu

"Those altering the numbers in Wajir East, Eldas and Tarbaj are after own political interests,"@bosiboriviews alisema.

@kiilundeti aliuliza, "The question is, can we ever get anything right as Kenyans?"

Akithibitisha kukamatwa kwa machihfu hao, kamishna wa kaunti ya Wajir Lyford Kibaara alisema walihusika katika kuongeza idadi ya watu katika lokesheni zao.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved