logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Tanzia! Aliyekuwa mwenyekiti wa TLB Hassan Kamwaro aaga dunia

Tanzia! Aliyekuwa mwenyekiti wa TLB Hassan Kamwaro aaga dunia

image
na

Burudani02 October 2020 - 03:02
KAMWARO
Aliyekuwa mwenyekiti wa bodi la Leseni za uchukuzi nchini TLB Hassan Ole Kamwaro ameaga dunia.

Kamwaro amekuwa akiugua saratani, na alifariki akipokea matibabu katika Mercy Hospital,mjini Oklahoma Marekani.

Kamwaro amekuwa akiugua saratani ya umio (koo) na alikuwa amesafiri Amerika kwa matababu zaidi. Mwanawe Jedida Kamwaro alithibitisha kifo chake siku ya Jumatano. Mwaka 2010, aliyekuwa rais Mwai Kibaki alifutilia mbali uteuzi wa Wilfred Lengei na kisha kumtaja Kamwaro kama mwenyekiti wa TLB.

Mwaka 2012, Kibaki alimteua Mhandisi Joseph Kamau kusimamia bodi ya TLB kuchukuwa nafasi ya Kamwaro.

Kamwaro alimuoa Eunice Sission mwaka 2012 katika hafla ya kibinansi iliyohudhuriwa na viongozi wa eneo analotoka pekee yao.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved